Kocha wa Arsenal – Mikel Arteta ameweka wazi kuwa wiki ijayo itaamua hatma ya kikosi hicho kwa msimu huu.
Arsenal wapo katika hali mbaya kwenye EPL msimu huu wakiwa wameshinda mchezo 1 kati ya 10 iliyopita na wanashika nafasi ya 15 kwenye msimamo wa EPL.
Arteta atakuwa mwenyeji wa Frank Lampard wakati Arsenal itakapowakaribisha Chelsea leo usiku. Baada ya mchezo huu, Arsenal watachuana na Brighton pamoja na West Brom. Hizi ni timu 2 zilizopochini ya Arsenal kwenye msimamo wa EPL.
Bila kupindisha maneno, Mikel Arteta amesema “Sina visingizio. Siku 7 au 8 zijazo zitakuwa za muhimu, zitatuonesha ni wapi tunaelekea kwenye Premier League.
“Nimekuwa muwazi tangu mwanzo kwamba tunapoteza michezo. Ni jukumu langu kusuluhisha hilo, bila kujali kitu chochote ni sisi tunaojianguasha wenyewe na ni sisi tunaopaswa kubadili hilo.”
Siku ya Jumatano, kocha wa West Brom – Sam Allardyce aliwataja Arsenal kama timu wanayoshindana nayo kwenye nafasi za kushuka daraja msimu huu. Kwamba haoni tofauti ya timu yake na Arsenal.
Kuelekea kwenye mchezo huu, Frank Lampard aliwaumiza Arsenal hapohapo Emirate msimu uliopita na Chelsea wamepoteza mchezo 1 pekee kati ya 9 waliyocheza dhidi ya Arsenal.
Hali itakuaje leo usiku. Ni Arteta au Lampard kuendelea alipoishia?
VUNA SHEA YAKO YA 230,000,000TSH NA UFURAHIE MSIMU HUU WA SIKUKUU!!!
Kupitia Kasino ya Mtandaoni ya Meridianbet, jiwekee nafasi ya kupata shea yako ya 230,000,000Tsh kupitia mchezo wa Secret Santa. Hakika hutojutia kufurahia msimu huu wa sikukuu ukiwa katika nyumba ya mabingwa ya Meridiabet. Unasubiri nini???



warda
Hapa arteta inabidi ajitahidi sana la sivyo atashika mkia
Adelta
Jamani hadi huruma aongeze juhudi atashinda
Rahmal
Dar anatakiwa aongeze juhudi atapata ushindi
Lydia Emmanuel Magoti
Daa Arteta anakazi kubwa sana
Ernest Kimeru
December siku zote inakuwa ngumu kwa Arsenal alkini msimu huu Arteta amekaa pabaya sana
Latifa juma mohamed
Duuh arteta ana kazi kubwa Sana.
Salma ngende
Waongeze juhudi
Issa
Arteta ajipe kipind
Saupha mohamed
Wapambane
Sarah
Arteta wajipange wapambane ili waweze kupata ushindi
Hopemwaikuka
Jamanii
Tatu
Wajipange upyaaa