Chelsea Kumfata Aubameyang, Barcelona wapo Tayari Kumuuza.

Chelsea wana uhakika wa kumsajili mshambuliaji wa Barcelona Pierre-Emerick Aubameyang, kwa mujibu wa ripoti.

The Blues wanasaka mshambuliaji mpya kabla ya dirisha kufungwa Septemba 1 baada ya kumuuza Timo Werner kwa RB Leipzig na kumruhusu Romelu Lukaku kuondoka kwa mkopo kwenda Inter Milan.

Chelsea imekuwa na sajili nyingi msimu huu wa joto huku Raheem Sterling, Marc Cucurella, Kalidou Koulibaly, Carney Chukwuemeka na Gabriel Slonina wakihamia Stamford Bridge.

Bado wanaonekana kupwaya katika maeneo kadhaa huku timu ya usajili sasa ikiweka juhudi yao yote kupata mshambuliaji mpya haraka iwezekanavyo.

Aubameyang, ambaye aliondoka Arsenal na kwenda Barcelona kwa uhamisho wa bure mwanzoni mwa mwaka huu, ameibuka kama shabaha yao kuu katika nafasi hiyo.

Chapisho la Uhispania la Cadena COPE linadai kwamba mauzo ya Aubameyang kwa Chelsea ‘yamepamba moto’ huku Chelsea na Barcelona ‘tayari kufanya mazungumzo’ kumnunua mchezaji huyo wa kimataifa wa Gabon.

Licha ya mabishano kuhusu kuondoka kwake Arsenal, takwimu za Aubameyang za ufungaji zimekuwa zikionekana kuwa nzuri kwa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 33 akiwa kafunga mabao 92 katika mechi 163 alizoichezea The Gunners.

Alionyesha uwezo mzuri akiwa na Barca msimu uliopita pia akiwa na mabao 13 katika mechi 23 lakini ripoti hiyo inaeleza Aubameyang akiwa kwenye ‘njia ya kuondoka’ Camp Nou huku miamba hao wa Catalunya wakitaka kuuza baadhi ya wachezaji wao kabla ya kusajili wachezaji wengine zaidi.

Acha ujumbe