Chelsea, PSG Katika Vita ya Hakimi.

 

Klabu ya Chelsea imetoa ofa sawa na ile ya Paris Saint-Germain ya pauni milioni 56.1m (€ 60m) kwa beki wa pembeni wa Inter Milan Achraf Hakimi.

 

Majarida mbalimbali nchini Italia yanaripoti kwamba Inter inaweza kuwa wazi zaidi kwa pendekezo la Chelsea kwa sababu ya hamu ya klabu ya Italia kwa Emerson Palmieri na Andreas Christensen.

Inter ingependa kumsajili beki Emerson Palmieri kwa mkopo wakati Chelsea ingependelea kumtoa moja kwa moja kwa mkataba wa kudumu.

Ofa ya The Bluez kwa Hakimi bado inaonekana kuwa chini ya dau la Inter Milan. Wameweka dau la chini la beki huyo wa Morocco kuwa pauni milioni 68.8 (€ 80m).


WEKA PESA KUPITIA DUKANI MERIDIANBET!

Chukua namba yako ya akaunti na kiasi cha pesa unachotaka kuweka, sogea kwenye duka lolote la Meridianbet lililo karibu nawe utasaidiwa kuweka pesa.

Weka Pesa Meridianbet

WEKA PESA

Acha ujumbe