Manchester City imefanikisha usajili wa kiungo mshambuliaji Rayan Cherki kutoka Olympique Lyonnais ya Ufaransa kwa mkataba wa miaka mitano mwezi huu, yakiwa ni maandalizi kuelekea kuanza kwa michuano ya Kombe la Dunia la Vilabu.

Maelezo ya kifedha ya mkataba huo hayakuwekwa wazi, lakini vyombo vya habari vya Uingereza viliripoti kuwa City ililipa takriban euro milioni 40 (dola za Marekani milioni 45.70) kwa mchezaji huyo wa Ufaransa mwenye umri wa miaka 21.
Cherki alikuwa na msimu wake bora zaidi akiwa na Lyon mwaka 2024-25, akifunga mabao 12 na kutoa pasi za mabao 20 katika mashindano yote.

“Hii ni ndoto kwangu. Kusema kweli, kujiunga na klabu kama Manchester City ni nafasi kubwa ya kufika hatua ya mbele katika maisha yangu ya soka na ni jambo la pekee sana,” Cherki alisema katika taarifa.
“Nimefanya kazi kwa bidii maisha yangu yote. Napenda mchezo huu na nasubiri kuendeleza ujuzi wangu hapa Manchester chini ya Pep Guardiola na benchi lake la ufundi.”
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa
“Nisingeondoka Lyon bila kuona mipango sahihi kutoka Manchester City, kila kitu hapa City kinaonyesha kuwa naweza kuendeleza mchezo wangu na kusaidia timu kufanikiwa katika siku zijazo. Ninasubiri wakati ufike ili niweze kuwaonyesha mashabiki wa City ninachoweza kufanya.”

Mchezaji huyo wa kimataifa wa Ufaransa ambaye hivi karibuni amecheza mechi za timu ya taifa, anaweza kucheza kama kiungo mshambulia pamoja na winga wa kulia. Alifunga mabao katika mechi zote mbili za robo fainali ya Europa League ambapo timu yake ilipoteza kwa jumla ya mabao 7-6 dhidi ya Manchester United.
Mkurugenzi wa michezo wa Manchester City, Hugo Viana, pia alionyesha kuridhika kwake na usajili huo.
“Yeye ni mchezaji ambaye wapelelezi wetu wamemuangalia kwa muda mrefu, na sote tumevutiwa na ujuzi wake pamoja na ubunifu. Nina hakika mashabiki wetu watakuwa na shauku ya kumuona akicheza,” alisema Viana.

Manchester City itaanza kampeni yake ya Kombe la Dunia la Vilabu Juni 18 dhidi ya timu kutoka nchini Morocco, Wydad AC, ikifuatiwa na mechi dhidi ya klabu ya Falme za Kiarabu, Al-Ain, na kisha Juventus.

