Mchezaji wa klabu ya Juventus Federico Chiesa amethibitisha kubakia na klabu na anatarajiwa kukabidhiwa jezi namba 10 baada ya kuondoka kwa mchezaji Paulo Dybala.
mchezaji huyo wa kimataifa amekuwa na msimu mzuri chini ya Massimiliano Allegri kwenye dimba la Turin kufuatiwa kuonyesha kiwango bora kwenye mashindano ya Euro 2020 kwenye majira ya kiangazi yaliopita. Lakini kila kitu kilisimama ghafla mwezi January, baada ya kusumbuliwa na maumivu ya goti.

Kwasasa Federico Chiesa anajiuguza majeraha yake, na inatarajiwa kuwa mpaka majira ya mvuli atakuwa amepona na kurejea uwanjani.
Kulingana na taarifa za Gazzetta dello Sport, juventus wamejikita zaidi kutafuta mchezaji ambaye watamwamini kumpa namba 10, na Chiesa ameoneka ni mtu sahihi kuweza kuva jezi hiyo kwa sababu za kibiashara, lakini kimfumo na mbinu hawezi kucheza namba 10.
Federico kiasili ni winga na sio kiungo mshambuliaji wala mshambuliaji wa kati kama Roberto Baggio na Alessandro Del Piero, licha ya kwanba amefanya kazi na Carlos Tevez na Paul Pogba.
Una Kila sababu ya kufurahia wiki yako na kutengeneza mwaka huu uwe wa faida zaidi katika kasino zetu za mtandaoni za meridianbettz. Mchezo wa Zeus Ancient Fortunes unakuongoza kutekeleza hilo.


