Chris Bryant: Abramovich Hapaswi Kumiliki Klabu ya Chelsea

Mbunge wa chama Labour Chris Bryant amelitaka bunge la nchini Uingereza kutomruhusu tena bilionare wa kirusi Roman Abramovich kumiliki klabu ya Chelsea kutokana na mgogoro uliopo kati ya Ukraine na Urusi.

Roman Abramovich alinunua klabu ya Chelsea mwaka 2003, na tokea hapo ameisaidia klabu hiyo kuchukua makombe yote ambayo klabu hiyo imewashiriki, Pia Abramovich alishawai kuzuia kuingia nchini Uingereza baada ya kuvuja kwa majina ya warusi waliokuwa na pesa haramu na utakatishaji na wafanya uhalifu wakubwa mwaka 2019.

Chris Bryant

Chris Bryant akiwa bungeni alinukuliwa akisema, kwenye nyaraka zilizovuja mwaka 2019 zilionyesha Abramovich akiwa sehemu ya warusi ambao watakatishaji pesa na kufanya vitendo vya kiarifu, ambao wanauhusiano wa moja kwa moja na serikali ya Urusi.

“Sasa ni miaka 3 imepita na bado ametoa ushirikiano hafifu, hakika Abramovich hapaswi kumiliki klabu ya mpira wa miguu kwenye nchi hii, tunapaswa kushirikilia mali zake, ikiwemo nyumba yake yenye thamani ya  £152milion na kuhakikisha tunakomesha wote wanaohusika na vitendo vya kiaharifu.” Chris Bryant aliongezea

Roman Abramovich alinyang’anywa uraia wa nchini Uingereza na kuzuia kuingia kwenye nchi hiyo kwa muda wa mika mitatu, na kwa sasa anamiliki uraia wa nchini Israel na Ureno.


SHINDA IPHONE 12 NA KASINO YA AVIATOR

Meridianbettz na Aviator wanakupa mchongo wa kuibuka na iPhone 12 katika kasino ya Aviator itakayodumu kwa siku 7. Kuwa rubani wa Aviator na ujishindie!

tetesi, Tetesi za Soka Barani Ulaya., Meridianbet

SOMA ZAIDI HAPA

Acha ujumbe