Erik Kuitazama United Live Jumapili Hii.

Watoto wa mjini wanasema, “tatizo ni muda”. Erik Ten Hag hataki kupoteza hata sekunde kwenye mchakato wa kuisuka upya Manchester United.

Baada tu ya kumaliza msimu na Ajax, Ten Hag alihamishia mawazo na nguvu zake zote kule Old Trafford akitazamia kuanza kazi rasmi baada ya msimu huu kutamatika. Erik hajapoteza muda, inataarifiwa kuwa ameshatua Uingereza na yupo jijini London toka jana mchana.

Manchester United ilimpatia ndege binafsi Ten Hag na Mitchell Van der Gaag ambaye anatarijiwa kutangazwa kama kocha msaidizi kule Old Trafford. Kwa sasa, wawili hawa wapo kwenye ofisi za makao makuu ya United kule London wakiendelea na mipango ya kuisuka United mpya.

Wakati hili likiendelea, Manchester United wataitupa karata yao ya mwisho msimu huu kwenye mchezo dhidi ya Crystal Palace kule Selhurst Park wikiendi hii. Huu ni mchezo ambao, Erik anatarajiwa kuwepo uwanjani hapo akiitizama kwa ukaribu zaidi timu anayokwenda kuiongoza mara tu baaada ya mchezo huo kutamatika.


TENGENEZA FAIDA NA ZEUS ANCIENT FORTUNES

Una Kila sababu ya kufurahia wiki yako na kutengeneza mwaka huu uwe wa faida zaidi katika kasino zetu za mtandaoni za meridianbettz. Mchezo wa Zeus Ancient Fortunes unakuongoza kutekeleza hilo.

tetesi, Tetesi za Soka Barani Ulaya., Meridianbet

CHEZA HAPA

Acha ujumbe