Eymael Atua Bongo

LUC Eymael, Kocha Mkuu wa Yanga leo ametua nchini Tanzania akitokea nchini Ubelgiji alikokuwa kwa ajili ya mapumziko ya lazima yaliyotokana na Virusi vya Corona.

Eymael ametua Uwanja wa Kimataifa wa Julius Nyerere na kupokelewa na baadhi ya Waandishi wa Habari ambao walikuwepo hapo.

Licha ya taarifa zake za kurejea leo kuwa wazi hakukuwa na mwakilishi yoyote wa Yanga ambaye alikuwa alikuwepo uwanjani hapo.

Kocha huyo anatarajiwa kuungana na wachezaji wake kesho, Shinyanga ambao wamekwenda huko kujiandaa na mchezo dhidi ya Mwadui FC utakaochezwa Juni 13.

Habari zinaeleza kuwa majukumu yalikuwa mengi kwa viongozi wa Yanga siku ya leo.

“Kuna mmoja amepewa likizo na wengine wapo na timu kwenye msafara hivyo kesho mambo yatakuwa sawa,” ilieleza taarifa hiyo.

26 Komentara

    Karudi awafundishe vyema wachezaji wake ili timu ifanye vizuri ipande viwango

    Jibu

    Yaani vyura fc bwana kocha ndo kaingia leo ha haaaaaa#meridianbettz

    Jibu

    Yanga kwa sasa hawana jipya..nawashauri wajipange upya

    Jibu

    Hii inamaana gani, kocha anarudi bila ata mapokezi??!! Mambo ya Bongo haya

    Jibu

    Duuh bongo noma sana

    Jibu

    Bora amerudi mana vijana walijiachia sana mpaka uzitu umeongezeka

    Jibu

    Duh hii Nina Sana jmn anarudi ata mapokezi hakunaaπŸ€”

    Jibu

    Duh hii noma Sana jamani anarudi bila ya mapokeziπŸ€”

    Jibu

    Afadhalii karudii ili wachezajii waongeze bidii zaidi

    Jibu

    Duh kazi ipo

    Jibu

    Kocha mahiri sana

    Jibu

    Sio kuwafundisha tu kuchukua ubingwa kabic yanga ya wanachi

    Jibu

    utopolo janja janja nyingi si hivyo katumiwa tickets katua nnchini

    Jibu

    Ahsante kwa taarifa

    Jibu

    Karibu kwenye timu yako mbovu mjiandae vipigo tu mwanzo mwisho

    Jibu

    Karibu tena bongo naona umekuwa mwenyeji ndio mana ukupokelewa

    Jibu

    Ni habar njema kwa wapenzi wa jangwan na wapenda soka thnks meridian bet kwa update za michezo

    Jibu

    Karibu tuanze mapinduzi yetu tupondue meza kombe lije nyumbani jangwan

    Jibu

    Habar njema kwetu wanayanga

    Jibu

    Habari njema kwa wenye chama lao

    Jibu

    Araf akapanda daladala airport pale kuelekea kkoo jangwani

    Jibu

    Karibu bongo eymael jangwani ndo kwako sasa .

    Jibu

    Duu noma Sana kocha katua ata mapokez mazuri hamna haya karibu kwenye timu yako mbovu upambane nayo

    Jibu

    Karibu sana

    Jibu

    Karudi kuendeleza ushindi au kufungwa

    Jibu

    Kalibu kumalizia ligi.

    Jibu

Acha ujumbe