FA Cup : Ratiba ya Robo Fainali.

 

Vigogo wa EPL, Klabu ya Liverpool, Chelsea na Manchester City zimekwepana katika droo ya robo fainali ya FA Cup iliyofanyika hapo jana.

 

Chelsea itaelekea ugenini kuvaana na Middlesbrough ambayo imefanikiwa kuwaondoa Tottenham na Manchester United katika hatua za awali.

Southampton watakuwa wenyeji wa Manchester City na Liverpool watacheza na mshindi kati ya Nottingham Forest na Huddersfield Town, ambazo zitacheza raundi ya tano Jumatatu.

Crystal Palace itacheza na Everton katika mechi nyingine baada ya vijana wa Frank Lampard kuwafunga Boreham Wood 2-0 mabao mawili yaliyofungwa na Salomon Rondon.

Mechi hizo zitachezwa kati ya Ijumaa, Machi 18 na Jumatatu, Machi 21.

Droo Kamili ya Robo Fainali ya FA Cup:

Middlesbrough vs Chelsea

Southampton vs Manchester City

Crystal Palace vs Everton

Nottingham Forest/Huddersfield Town vs Liverpool.


KASINO YA MTANDAONI: EMOTICOINS SABABU YA KUVUNA ZAIDI.

Haijawahi kuwa rahisi hivi kwenye safari yako ya kuvuna mkwanja, kasino maridhawa ya meridianbettz inakuletea mchezo wa Emoticoins unaokupa nafasi ya kufanya safari yako kuwa rahisi zaidi. Wakati ni wako nafasi ni yako na Emoticoins.

senegal, Senegal Mabingwa AFCON 2021., Meridianbet

CHEZA HAPA.

Acha ujumbe