Vigogo wa EPL, Klabu ya Liverpool, Chelsea na Manchester City zimekwepana katika droo ya robo fainali ya FA Cup iliyofanyika hapo jana.
Chelsea itaelekea ugenini kuvaana na Middlesbrough ambayo imefanikiwa kuwaondoa Tottenham na Manchester United katika hatua za awali.
Southampton watakuwa wenyeji wa Manchester City na Liverpool watacheza na mshindi kati ya Nottingham Forest na Huddersfield Town, ambazo zitacheza raundi ya tano Jumatatu.
Crystal Palace itacheza na Everton katika mechi nyingine baada ya vijana wa Frank Lampard kuwafunga Boreham Wood 2-0 mabao mawili yaliyofungwa na Salomon Rondon.
Mechi hizo zitachezwa kati ya Ijumaa, Machi 18 na Jumatatu, Machi 21.
Droo Kamili ya Robo Fainali ya FA Cup:
Middlesbrough vs Chelsea
Southampton vs Manchester City
Crystal Palace vs Everton
Nottingham Forest/Huddersfield Town vs Liverpool.
Haijawahi kuwa rahisi hivi kwenye safari yako ya kuvuna mkwanja, kasino maridhawa ya meridianbettz inakuletea mchezo wa Emoticoins unaokupa nafasi ya kufanya safari yako kuwa rahisi zaidi. Wakati ni wako nafasi ni yako na Emoticoins.