Bao pekee la Yanga lililofungwa na Feisal Salum kwenye mchezo wa jana limewanyima kitita cha Mil 20 nyota wa Tanzania Prisons.

Mchezo huo wa ligi kuu ulipigwa jana jumapili kwenye Uwanja wa Mkapa, Dar ambapo Yanga walifanikiwa kuibuka na ushindi wa bao 1-0 lililofungwa dakika ya 89.
Kabla ya mchezo huo, wadhamini wa Tanzania Prisons, Silent Ocean waliahidi kitita cha Mil 20 kwa wachezaji na benchi la ufundi endapo watapata ushindi kwenye mchezo huo.
Baada ya ushindi huo Yanga wanarejea kileleni mwa msimamo wa ligi baada ya kukusanya pointi 35 baada ya kucheza mechi 14.

