Mayele: Feisal ni Kama Thiago Alcantara

Mshambuliaji wa Young Africans SC Fiston Mayele ambaye pia ni Raia wa DR Congo amemfananisha kiungo wa Yanga Feisal Salum “Fei Toto” kama Thiago Alcantara ambaye ni kiungo wa Liverpool.
Mayele: Feisal ni Kama Thiago Alcantara
Thiago Alcantara

Mayele ambaye jana alikuwa na mchezo mzuri, aliweza kufanga hat-trick yake ya kwanza kwenye Mashindano ya Klabu Bingwa, akiweka rekodi baada ya kupita miaka nane bila mchezaji yeyote wa Ligi ya Tanzania kufunga hat-trick, mara ya mwisho ilikuwa ni mwaka 2014 Mrisho Ngasa alifunga Hat-trick kwenye hatua ya awali.

Mayele: Feisal ni Kama Thiago Alcantara

Katika ukurasa wake wa Twitter Mayele aliposti picha akiwa yeye na Feisal huku akisindikiza na maandishi “Thiago Alcantara” akimaanisha kwamba Fei ni kama Kiungo wa Liverpool Alcantara.

Mayele: Feisal ni Kama Thiago Alcantara

Yanga SC ilianza vizuri kwenye mechi yake ya kwanza kwa kuwachalaza vibaya Zalan FC ya Nchini Sudan Kusini mabao 4-0 huku Fiston akizama nyavuni mara tatu na Feisal akizama mara moja.

 

View this post on Instagram

 

A post shared by Young Africans Sports Club (@yangasc)

Mechi ya pili itampaswa Yanga asifungwe goli zaidi ya 4, ili aweze kuendelea kwenye hatua ya Kwanza ambapo kama atafanikiwa kufuzu atakutana na mshindi katika ya AL Hilal ya Sudan au St George FC kutoka Ethiopia.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.