Shirikisho la Mpira Duniani (FIFA) imezifungia Zimbabwe na Kenya kushiriki na kujiusisha na maswala yeyote ya kimpira kwa muda usiofahamika hapo jana baada ya serikali kuingilia uendeshaji wa vyombo vyao vya soka vya kitaifa.

Zimbabwe ilipigwa marufuku baada ya Tume yake ya Michezo na Burudani inayoendeshwa na serikali kukataa kuachia udhibiti wa Chama cha Soka cha Zimbabwe na kurejesha uongozi wa shirikisho hilo.
Maafisa wa ZIFA waliondolewa ofisini mwezi Novemba kwa madai ya ufisadi.
Kenya ilipigwa marufuku baada ya wizara yake ya michezo pia kuwaondoa viongozi wa shirikisho la soka na kuwashutumu kwa ufisadi. Rais wa soka wa Kenya Nick Mwendwa anakabiliwa na mashtaka ya uhalifu.
Rais wa FIFA Gianni Infantino alitangaza marufuku hiyo wakati Baraza la FIFA lilipokutana kwa muda mfupi kwa mkutano wa video siku ya Alhamisi
Hii maana timu za taifa za Zimbabwe na Kenya na vilabu haviwezi kucheza katika mashindano yoyote ya kimataifa. Pesa kutoka FIFA pia zimezuiwa.
Meridianbettz na Aviator wanakupa mchongo wa kuibuka na iPhone 12 katika kasino ya Aviator itakayodumu kwa siku 7. Kuwa rubani wa Aviator na ujishindie!


