PSG wamekunjua dau la paundi milioni 21.5 kama ofa ya kumnasa nyota wa Everton Idrisa Gueye, lakini bado Everton wanaonekana kuhitaji bunda kubwa zaidi, angalau mara mbili ya dau lao kwa mujibu wa Sky Sports!
Mabingwa hawa wa Ufaransa wanahitaji kutatua shida ya Viungo wakiwa wamekumbwa na seke seke la majeruhi kwenye klabu hiyo huku wakikosa mbadala wa kudumu wa Marco Verratti. Wamemtupia macho nyota huyu, Gueye ambaye kwa sasa yupo kwenye fomu nzuri katika Ligi Kuu ya Uingereza.
Wakati huo Everton, ambao wanatajwa kutaka dau kubwa zaidi ya ofa iliyopo mezani, wao wapo sokoni wakimwinda mshambuliaji baada ya Cenk Tosun kuwa katika kipindi kigumu. Wakati wakitarajia kumnasa Richalison, inadaiwa kuwa Everton hawataweza kumuachia nyota wao hadi wahakikishw wamepata mbadala wake.


Isha
Safi sana iyo ni fulsa
Mariam mtandama
Safi
Povel tz
Habar njema