Aliekua Raisi wa Olimpique Marseille Afariki Dunia

Pape Diouf ndie alikua Raisi wa kwanza Mweusi wa klabu zinazo shiriki ligi kuu nchini Ufaransa. Raisi huyo raia wa taifa la Senegali aliongoza Marseille kati ya mwaka 2005 hadi 2009 kipindi ambacho timu hiyo ilichukua nafasi ya pili ya ligi kuu na kushiriki fainali za kombe la Ufaransa mara mbili. Na ulipofika mwaka 2010 walichukua ubingwa wa ligi baada ya miaka 18.

Pape Diouf enzi za uhai wake

Pape Diouf amefaliki akiwa na umri wa miaka 68 baada ya kukutwa na maambukizi ya Virusi Korona (COVID19). Timu hiyo imeripoti “Pape atabaki mioyoni mwa wana Marceille milele, kama moja ya watu walio itengeneza historia ya timu yetu” Marseille walipost ujumbe huo kwenye kurasa zao za mitandao ya jamii.

Bodi ya mchezo wa mpira wa miguu wa kimataifa ya nchini Ufaransa (L.F.P)  imesema “ Tumepoteza  Muandishi, Wakala, Na Raisi wa Olympique Marseille, Pape amehudumu maisha yake yote kwenye mpira wa miguu, kwetu alikua ni mwanachama wa LFP tangu Septemba 2007 mpaka  juni 2009 Tutamkumbuka Pape kama muhisani  na kiongozi mwenye Tija ”

Pape Diouf akiwa na Djibril Cisse

Mchezaji wa zamani wa Liverpool Djibril Cisse aliwahi kuitumikia Marseille kipipindi ambacho Pape anaiongoza timu hiyo amesema. “Leo mota wa Ufaransa umepoteza mtu muhimu, Maumivu yangu ni makubwa mno pumzika kwa amani”

 

 

3 Komentara

    Hongera sana.

    Jibu

    R.I.p

    Jibu

    R.I.P

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.