Beckham Amewapania Messi na Ronaldo Kutua Miami

Staa aliyepata umaarufu sana kupitia soka ambaye kwa sasa anamiliki klabu yake ya Inter Miami, David Beckham amepania kuwanasa mastaa wanaotikisa ulimwengu wa soka Lionel Messi na Cristiano Ronaldo kutua klabuni kwake.

Staa huyu ambaye amewahi kukipiga pale LA Galaxy, anafanya maandalizi ya timu yake kuingia rasmi kwenye soko la soka kwenye ligi inayofahamika kama Major League Soccer msimu ujao. Kuna taarifa zinazotaja mipango yake ya usajili kuelekea shughuli iliyopo mbele yake!

Beckham ambaye pia amewahi kuwa staa wa Manchester United, Real Madrid amekuwa akiweka wazi matamanio yake ya kuwanasa Christiano Ronaldo aliyepo Juventus na Lionel Messi fundi wa Barcelona licha ya kutambua ugumu uliopo kumuondoa Messi Barcelona au kuwashawishi Juventus kumuachia Ronaldo.

Akiweka wazi mipango ya klabu yake na kuwazungumzia mastaa hawa anasema kuwa kila mtu nhuwa na mipango, orodha ya mambo ambayo anahitaji kuyatimiza. Anasema ukiwaangalia Leo na CR7 wanavyocheza unawezaona kama wanakaribia kumaliza soka lao, lakini yeye haoni hivyo. Licha ya kuwa wanacheza soka katika levo kubwa kabisa ni ngumu kuona wakiziacha klabu zao lakini anasema wataangalia, hauwezi jua nini kinaweza kutokea katika soka.

Beckham Amewapania Messi na Ronaldo Kutua Miami
Ndoto ya Beckham ni Messi na Ronaldo Kutua Miami

2 Komentara

    Gud news

    Jibu

    Hao ndo mabingwa wa dunia

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.