Eze Azidi Kung'ara, Arteta Asema Bado Kuna Mengi Zaidi

Mikel Arteta, ameonyesha imani kubwa kwa Eberechi Eze baada ya kiungo huyo kufunga bao lake la kwanza kwa klabu hiyo katika ushindi wa 2-0 dhidi ya Port Vale kwenye Kombe la Carabao, Jumatano usiku.

Eze alitikisa nyavu dakika ya nane tu katika uwanja wa Vale Park, akionyesha makali yake mapema. Hata hivyo, Arsenal walihangaika kutengeneza nafasi safi dhidi ya wenyeji wao wa Ligi ya Daraja la Kwanza, hadi Leandro Trossard alipoingia na kufunga bao la pili dakika ya 86, kuhitimisha ushindi.

Eze Azidi Kung'ara, Arteta Asema Bado Kuna Mengi Zaidi

Bao hilo lilikuwa la kwanza kwa Eze tangu atue Arsenal kwa dau la pauni milioni 60 kutoka Crystal Palace, na usiku huo alionekana kuwa mchezaji hatari zaidi katika safu ya ushambuliaji ya The Gunners.

Arteta alisema “Alicheza katikati dhidi ya timu iliyojipanga 5-4-1, wakibanana sana. Si rahisi kupata nafasi, lakini Eze ana uwezo mkubwa. Alifunga na pia alifanya matukio mengine matatu au manne ya hatari.”

Kocha huyo aliongeza kuwa Eze bado anahitaji muda zaidi kucheza na wachezaji wenzake ili kuelewa muda na mizunguko ya pasi, akisisitiza kuwa matukio kama hayo yatakuwa ya kawaida na yenye tija zaidi kwa timu.

Katika mechi hiyo, Eze alianza kushambulia kutoka upande wa kushoto, lakini tayari ameshachezeshwa katika nafasi mbalimbali na Arteta katika mechi tano alizocheza hadi sasa.

Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa.

Eze Azidi Kung'ara, Arteta Asema Bado Kuna Mengi Zaidi

Arsenal walitumia majira ya kiangazi kuongeza kina katika kikosi chao ili kuhimili mashindano mengi msimu huu. Hali hiyo ilijidhihirisha kwenye orodha ya wachezaji, ambapo Arteta alifanya mabadiliko tisa kutoka kikosi kilichotoka sare ya 1-1 dhidi ya Manchester City, lakini bado akawasilisha kikosi imara.

Kepa Arrizabalaga alicheza mechi yake ya kwanza langoni, Christian Nørgaard alianza kwa mara ya kwanza kiungo, na Bukayo Saka alicheza kwa dakika 60 baada ya kupona majeraha ya msuli wa paja. Arteta alisema ana maamuzi mengi ya kufanya kabla ya safari ya Jumapili kuelekea Newcastle.

“Tunachotakiwa kufanya ni kutengeneza kiwango tunachotaka kwa wachezaji ambao hawajazoea kucheza pamoja,” alisema. “Kiungo kilikuwa tofauti kabisa, safu ya mbele pia. Lakini Max Dowman alikuja na kuungana haraka na timu.”

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.