Marouane Fellaini kukopesha klabu yake ya zamani ya Standard Liege ili kutoshushwa ligi daraja la nne. Klabu hiyo ya Ubelgiji tayari ilikuwa kwenye ukata mkubwa wa kifedha hata kabla ya janga la virusi vya Corona ambalo limezidisha hali kuwa mbaya zaidi.
Mnamo mwezi Aprili, Shirikisho la Soka la Ubelgiji lilikataa kuwapa Standard Liege leseni kutokana na klabu hiyo kudaiwa malipo ya mishahara kutoka kwa wachezaji. Klabu hiyo imewaomba wachezaji wake wa zamani kuwasaidia ili kujikwamua katika anguko la kiuchumi walilopo na vyombo vya habari vya Ubelgiji vinaripoti kuwa Fellaini atatoa mkopo wa Euro milioni 2.6 kwa klabu hiyo.

Nyota huyo wa zamani wa Everton na Manchester United, anaekipiga kwenye klabu ya Shandong Luneng kwasasa ameungana na kiungo wa BVB Axel Witsel kutoa mkopo kwa klabu hiyo. Witsel alicheza Standard Liege takribani michezo 1500 kwa zaidi ya miaka mitano kati ya mwaka 2006-11.
Nyota huyo wa Dortmund kwa kushirikiana na wawekezaji wametoa msaada wa Pauni milioni 1.3 na pia kuchangia asilimia 45 katika maboresho ya uwanja wa klabu, ambayo yamepangwa kufanyika katika miaka ijayo.
Mahakama ya Ubelgiji itatoa uamuzi juu ya hatma ya klabu hiyo tarehe 5 Mei na kwa mujibu wa Bladbe, klabu inahitaji kutafuta nyongeza ya angalau Euro milioni 12 ili kuendelea kuwepo katika ligi kuu kwa msimu ujao.


John mwakalosi
Nimeipenda hii kukumbuka ulikotoka na kusaidia pale penye uhitaji big up big boys
furahav
Nikwel lazma ukumbuke ulipotoka mana ipo cku utakwama utarudi tena.
Hidaya Mohammed
Ni vizuri kukumbuka ukipotoka!
Mwanaidi
Safii sana ndio inavyotakiwa👍
Mwajuma
Ameonyesha moyo waupendo hongera kwake😘
Hopemwaikux
Msahau kwao mtumwa big up kwao
Zainabu
Vizuri kwa kukumbuka ulipotoka
Rehema
Ni vizuri
samiah
Nyumbani ni nyumba htaka porini
Tatu
Safi sana
Samira
Mkataa kwao mtumwa big up💪💪
Salma
Ni wachache sana wanakumbuka walipotoka hongera
Neema hassan
Amefanya Jambo zuri Sana.