De Vrij Anafahamu Kuhusu Nia ya LaLiga Huku Uamuzi wa Mkataba wa Inter Ukikaribia

Beki wa Inter Milan Stefan de Vrij amefahamishwa kuhusu vilabu vya LaLiga na wakala wake anapofikiria iwapo ataongeza mkataba wake San Siro.

 

De Vrij Anafahamu Kuhusu Nia ya LaLiga Huku Uamuzi wa Mkataba wa Inter Ukikaribia

Huku dili la De Vrij likikamilika mwishoni mwa msimu huu, mabingwa wa Uhispania Real Madrid pamoja na wapinzani wao Atletico Madrid wametajwa kumtaka mchezaji huyo.

Inter watampoteza Milan Skriniar mwishoni mwa kampeni baada ya kufikia makubaliano ya awali ya mkataba na Paris Saint-Germain, na mlinzi mwenzake De Vrij anaweza kumfuata kupitia mlango wa kutokea.

Alipoulizwa kuhusu kutakiwa na klabu kubwa za Uhispania baada ya sare tasa hapo jana dhidi ya Sampdoria, De Vrij alisema: “Haya ni maneno kutoka kwa wakala wangu, najaribu kuzingatia kazi na uwanjani.”

De Vrij Anafahamu Kuhusu Nia ya LaLiga Huku Uamuzi wa Mkataba wa Inter Ukikaribia

Hata hivyo, matarajio ya mchezaji huyo wa Kimataifa wa Uholanzi kusalia Milan hayawezi kuondolewa, kwani aliongeza kuwa ana maelewano mazuri na klabu na wanazungumza na kukiwa na habari watagundua.

Inter sasa wako nyuma ya vinara wa Serie A kwa pointi 15, Napoli kufuatia kushindwa kwao kuisambaratisha Sampdoria, na De Vrij anakubali kwamba Scudetto imepotea katika kampeni hii.

De Vrij Anafahamu Kuhusu Nia ya LaLiga Huku Uamuzi wa Mkataba wa Inter Ukikaribia

“Pointi 15 mbali na Napoli ni nyingi sana. Kwa upande mmoja kuna Napoli ambayo inaenda kasi sana kwa kushinda kila mchezo, kwa upande mwingine ni sisi, ambao hatuwezi kuleta matokeo fulani nyumbani.”

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.