Winga wa kimataifa wa Ureno na mabingwa watetezi wa ligi kuu ya Italia klabu ya Ac Milan Rafael Leao ameakaribia kusaini mkataba mpya wa kuendelea kusalia ndani ya klabu hiyo.
Klabu ya Ac Milan inapambana kuhakikisha mchezaji Rafael Leao anasaini mkataba mpya na klabu hiyo kutokana na uwezo mkubwa ambao amekua akiuonesha mchezaji huyo. Klabu hiyo inapambana kumpa mkataba mchezaji huyo kutokana na ubora wake.
Klabu ya Ac Milan imekua ikiharakisha kuhakikisha mchezaji huyo anasaini mkataba mpya ndani ya Milan kutokana na ushindani mkubwa ambao umekua ukiletwa na vilabu mbalimbali barani ulaya ambao wamekua wakitaka saini ya mchezaji huyo.
Rafael Leao amekua kwenye kiwango cha hali ya juu ndani ya klabu ya AC milan na kufanikiwa mchezaji bora wa ligi kuu nchini Italia msimu uliomalizika, Kitu kilichomfanya kupandisha thamani ndani ya timu hiyo na kuvutia vilabu mbalimbali barani ulaya.
Ac Milan kupitia mkurugenzi wao Paulo Maldini wamekua wakizungumza juu ya na yao ya kuhitaji Rafael Leao abakie ndani ya klabu hiyo kwa kusaini mkataba mpya, Taarifa za ndani zinaeleza mchezaji huyo amekaribia kusaini mkataba mpya wa kuendelea kusalia ndani ya Milan kwa miaka mingine kadhaa.

