Ilikuwa kama utani pale klabu ya Liverpool ilipoonesha kuwa tofauti sana na huku kwetu mara baada ya kumshitaki mshambuliaji wake, Mohamed Salah baada ya kuendesha gari wakati anachati kwa simu yake ya mkononi!
Ilikuwaje?
Mo Salah alirekodiwa na baadhi ya mashabiki wa Liverpool akiwa katika foleni ambapo baadhi ya mashabiki hao walitaka kuzungumza naye ila yeye hakufungua kioo kabisa.
Akakataa na kuendelea kuchati huku akisogea taratibu na baada ya video hiyo kusambaa kwenye mitandao ya kijamii klabu yake ya Liverpool ikaripoti polisi juu ya tabia hiyo ya kuendesha huku anatumia simu yake!
Jeshi la Polisi jijini Liverpool, Uingereza likaanza kulifanyia uchunguzi sakata lake hilo! Leo hii Liverpool inasafiri kwenda kuumana na Crystal Palace, unaweka wapi karata yako?



Issa
Livepool ubaya huo
Povel
Gud news