Wiki ya 30 ya gemu za Ligi Kuu ya Uingereza (EPL) imeendelea kuonesha ushindani mkubwa sana huku ikiendelea kutoa picha ngumu ya nani hasa atatwaa taji hilo kwa miamba wawili waliopo kileleni!
Watabe Manchester City wameendelea kutawala kileleleni lakini wakiwa bado na hofu ya kuweza kupinduliwa wakati wowote kutokana na utofauti wa pointi moja tu. Bingwa huyu amejihakikishia kubakia kinara kwa wiki ya gemu ya 30 baada ya kumchapa Watford bao 3-1.
Hii wiki haikuwa ya Tottenham Hotspurs ambao walikubali kichapo kutoka kwa wenyeji wao, watakatifu wa Southampton. Kichapo cha bao 2-1 walichokipata Spurs kinawaacha wakiwa nafasi yao ile ile lakini wanatupwa nyuma kwa pointi 13 dhidi ya vinara Liverpool, sio rahisi sana kuondoa gepu hilo kwa mechi zilizobakia.
Liverpool ambaye alikuwa anaombewa njaa na City naye ameweza kubakiza gepu dogo la pointi baada ya kumchapa Burnley kwa bao 4-2 akiwa na matumaini huenda mambo yakabadilika na akarejea kuwa kinara.
Arsenal na Manchester United wote walikuwa wanataka kumaliza wiki hii wakiwa wanashikilia nafasi ya 4, Manchester United ambaye alikuwa hataki kumuachia Arsenal nafasi hiyoalikuwa anamuongoza Arsenal kwa yofauti ya pointi 1. Bahati haikumlalia vyema Man U ambaye amekubali kichapo cha bao 2-0 na kuteremka nafasi ya 5.
Chelsea naye alihitaji kupambana ili aweze kumg’oa Man United mtaa wa 4 kama angeshinda gemu dhidi ya Wolverhampton wakati Wolves wao wakiwa mtaa wa 7 walihitaji zaidi kuuhama mtaa huo wamuachie Chelsea! Hakuna aliyekuwa na bahati zaidi wakimaliza kwa sare ya 1-1, Wolves wakisalia mtaa wa 7!
Ligi inaendelea kuwa ya moto mnno, sio rahisi kutabiri moja kwa moja kuwa nani atakuwa wapi mpaka msimu unapokwisha.
Msimamo Baada ya Wiki 30 ya Mechi EPL
Furahav
Sikuzote ligi ya uingereza ni ligi bora sana duniani.