Virgil van Dijk amefunguka kuwa alizingatia mambo mengi kabla ya kuamua kujiunga na Liverpool. Mholanzi huyo pia alikuwa kwenye rada ya Manchester City lakini aliamua kuhamia Anfield mnamo Januari 2018.
Van Dijk anadai mtindo wa kucheza wa Waajili wake Liverpool ni baadhi ya mambo muhimu katika uamuzi wake. Vijana hao wa Jurgen Klopp walifikia fainali ya Ligi ya Mabingwa ndani ya miezi sita tangu kuondoka kwake kwa Pauni 75m kutoka Southampton.
“Kabla sijafanya uamuzi wa kuchagua Liverpool, niliangalia nyanja zote za vilabu; njia ya kucheza, wachezaji wa timu, hatma pia,” aliiambia BT Sport.
“Jiji, mashabiki, Wachezaji wenza kilikuwa ni sehemu ya kitu kikubwa ya kujiunga na Klabu…Nadhani Liverpool wakati huo nilipofanya uamuzi ilikuwa uamuzi sahihi na ni dhahiri kufikia fainali ya Ligi ya Mabingwa katika miezi sita yangu ya kwanza ilikuwa wazi ni bonasi kubwa na ilinisaidia sana katika ukuaji wangu.”
Tangu walipofungwa na Real Madrid huko Kiev Liverpool wamejijenga upya na kurejea kwa nguvu na kuwa mabingwa wa Ulaya mnamo Juni mwaka jana… Pia wako mbioni kushinda taji lao la kwanza la Premier league ikiwa msimu utaanza tena.
Gabriel
Kwel kabisa Virgil van dijk
Salma
Safi
Tahiya
Ni vzr kuwa na mapenzi na timu uichezayo
Ester mmakasa
Ni bora kawa muwazi na kaonesha mapenzi ya dhati na timu yake.
Adelta
Inapendeza kuwa na mapenzi na Tim yako
Lombo
iko poa
Ernest
One of the Best Defender on world football now.
Emmy cleopa
Vizur sana
Furahav
Beki kisiki.
Nasra
Nice
Shafii
Itakua alikua mashabiki wa Liverpool before
Povel
Yap anastail kwl kuwepo pale ni mtu sahh meridian bet tz#
mwakalosi
Best defender kwa sasa
Frank patrick
Vvd 💪
Adelta
Iko poa
Mariam mtandama
Safi
Rehema Dickson
Safi sana basi anastahili kuwepo Liverpool maana alikua na mapenzi kabla ata ajaenda kuitumikia Liverpool