“nilikua na furaha sana kurudi, nimerudi kuja kumalizia kazi niliyo iacha” Paul Pogba alirudi Old Trafford mwaka 2016 kwa Ada ya Pauni Milioni 89 ambayo ilikua ni rekodi mpya ya usajili ghali zaidi kwa wakati ule. Pogba anesema mama yake alimwambia kua arudi Manchester United baada ya kuondoka kilabuni hapo mwaka 2012.
Mwanasoka huyo Raia wa Ufaransa anaeye chezea pia timu ya taifa lake alijiunga na Juventus ama mchezaji huru mwaka 2012 baada ya kukosa namba katika kikosi cha kwanza cha timu ya Manchester United. Lakini licha ya kuhama Manchester United kama mchezaji huru, Pogba anasema Mama yake muda wote alikua ana sistiza swala la mwanandinga huyo kurudi Manchester United.

Pogba anasema moja ya kauli za mama yake ilikua ni ” Utaenda sehemu nyingine lakini ni lazima urudi”
“unawajua tena wakina mama waki n’gan’gania jambo lao aliniambia utarudi tu hapa usijali na aliniambia hayo nilivyotoka United na nikweli nimerudi”
Pogba hajaitumikia Manchester united tangu mwishoni mwaka mwaka 2019, na hii ni kutokana na majeraha yaliyo mkuta kuelekea mwishoni mwa mwaka 2019 na wakati Pogba anaelekea kupona na kutarajia kuitumikia Manchester United, Michezo inasimamishwa katika ligi mbali mbali kutokana na Janga la Korona (COVID19)


Aziza mushi
Asanten kwa makala.
Sadick
Kwa sasa anapotaka kuhama Man U ni uamuzi wa nani? siku zote fanya uamuzi unatoka moyoni mwako#meridianbettz
Povel
Gud news
Chiku
Imekaa poa sana