Paris Saint-Germain wametwaa ubingwa wa Ligi ya Ufaransa maarufu kama Ligue 1 ambao umemalizika kwasababu ya janga la Corona.
PSG walikuwa pointi 12 juu kwenye msimamo wa Ligue 1 ikiwa michezo 11 imesalia kumaliza baada ya ligi kusimama kama hatua za kuzuia kusambaa kwa Corona.
PSG wamepewa taji la Ligi baada ya Waziri Mkuu wa Ufaransa Edouard Philippe kutangaza hakuna matukio ya michezo yatakayoendelea katika nchi hadi Septemba.

Pointi moja kwa mchezo ndio mfumo uliotumika kuamua hatma ya msimamo wa Ligue 1.
Marseille, wakiwa nafasi ya pili, wamefuzu moja kwa moja kwenda Champions League wakati nafasi ya tatu Rennes ataenda kwenye hatua ya mtoanow.
Toulouse na Amiens wameshuhswa daraja kutoka ligi kuu. Lorient wametwaa ubingwa wa Ligue 2 na Lens watapanda daraja kwenda ligi kuu.
Klabu imesema “Tunapeleka kombe hili kwa watumishi wa afya na siku zote hao ndio mashujaa wakiwa mstari wa mbele”.
Mwenyekiti na Mkurugenzi Mtendaji wa PSG, Nasser Al-Khelaifi ameongeza kusema watumishi wa afya wamejitoa kwa wiki nyingi wanahitaji kuangalia kwa tofauti”.
Ameendelea: “Tunaelea na kuheshimu maamuzi yaliyotolewa na serikali ya Ufaransa kumaliza ligi. Kama serikali ilivyosema afya ni kipaumbele cha kila mtu.
“Katika waka ti mgumu, natumaini hili taji litaleta furaha kidogo kwa mashabiki wetu wote. Ni washukuru wote kwa maamuzi yenu kwano mmeisaidia PSG kuendelea kusonga.”



Ester jackson
Mcheza vizur hutuzwa
Samira
Wamestahili hili taji
Gabriel
Ila sio maamuz sahih wangecheza ata bila mashabiki ili tuone uhondo
Asia Abdy
Wahudumu wa afya wana mchango mkubwa sana hasa kipindi hiki cha Corona.hongera PSG kwa ushindi
Tahiya
Yaani ubingwa bila kusherehekea daah ili janga cjui litaisha lini mungu atulinde
JULIANA
Maamuzi yao no bomba
Ananiambtz
Hongera zao kwa ushindi PSG
Zainabu
Wanastahili kabisaaa hao watumishi wa afya nimeipenda hiyo….
Mathayo sonje
Ni jambo la msingi sana PSG wamefanya ni jambo la kuigwa na wengine pia.
Hamidu
Amestahili kuchukua ubingwa
Wahida
Bora walivyomaliza bwana mana Kurudi kucheza ni ngumu
Aziza moshi
Hayo ndo maamuz yalobaki baada ya ufaransa kusimamisha ligi kwasababu ya corona hongera kwa taji PSG
Neema juma
Kwa kweli afya ni kipaumbelee cha kila mtu
Furahav
Na nchi nyingine wanatakiwa wafanye hivyo itakuwa vzur
Agness
Hongera psg kwa ushindi mko vizuri
Theckla
PSG walistahili kuchukuwa ubingwa
Waziri
Hayo ndo maamuzi mazuri coz Corona nijanga la dunia zima
SADICK
Kongole PSG
Poveli liwongolo
Wamestail kwn ligi wametawala wao
Genia Sikaluzwe
Hongera psg kwa ushindi
Nasra
Hongera PSG