Kwa Cristiano Ronaldo, hakuna kitu kilionekana kwenda sawa kwenye mechi ya nusu fainali ya Coppa Italia dhidi ya AC Milan Jumamosi ya wiki iliyopita. Akikosa penati, mfululizo wa nafasi nyingi akipoteza na kiwango duni kwenye mchezo wa Nusu Fainali, kwa ujumla hakuwa kwenye ubora wake kwenye mechi ya nusu fainali ya Kombe la Italia dhidi ya AC Milan.
Ila kwa bahati nzuri nyota huyo mwenye Ballon d’Or 5, game ilimalizika kwa sare tasa (0-0) na Juventus akapata nafasi ya kutinga kwenye fainali ya Jumatano hii dhidi ya Napoli. Ronaldo sasa ana kila sababu ya kuingia katika Fainali ya kesho kupambana kutafuta taji lake la 30 kwa klabu na timu ya taifa.
Kama ilivyokuwa kwa wachezaji wengi waliocheza nusu fainali ya Coppa Italia, Ronaldo pia alionyesha dalili za kutokuwa fit baada ya kuwa nje ya dimba kwa zaidi ya miezi mitatu wakati wa janga la Corona. Nafasi yake ya kwanza kwenye Nusu Fainali ilianza kwa kukosa penati katika kipindi cha kwanza, ikiwa ni mara yake ya kwanza kukosa tangu Januari 2019.
Ronaldo pia alionekana kupata changamoto ya kujiweka katika maeneo sahihi kutoka kwenye nafasi yake ya kawaida kwenye winga ya kushoto kwenda katikati wakati wa kushambulia. Huku kukiwa na uwezekano wa Gonzalo Higuain kuendelea kukosekana kwenye mchezo wa fainali huko Roma, Ronaldo anatarajiwa kusimamishwa mbele wakati Juventus itakapo kuwa ikitafuta taji lake la 14 la Kikombe cha Italia.
Juventus inalenga kubeba taji lake la kwanza kati ya matatu inayowinda msimu huu (Trebble), wanashika nafasi ya kwanza kwenye msimamo wa Serie A, alama moja mbele ya Lazio na pia wanaangalia kupindua matokeo ya bao 1-0 dhidi ya Lyon katika mchezo wa pili wa raundi ya 16 kwenye Ligi ya Mabingwa.
Kwa upande wa Napoli bado pia wapo kwenye Ligi ya Mabingwa, na Jumatano hii watakuwa wanatafuta kushinda Kombe lao la sita la Italia. Mshambuliaji Dries Mertens katika Nusu fainali aliweka kambani na kuandika rekodi ya mabao mengi katika historia ya klabu ya Napoli..Kesho ataendeleza kuweka rekodi??
Lydia Emmanuel Magoti
Safii itapendeza kwasababu Ronaldo anajua nn anafanya
Povel
Cr7 mchezaj mkubwa sitegemeh Kama hatafany makosa Tena Kama yale thnks meridian bet kwa update za michezo na burudani
Rehema
Iko vizuri
Theckla
Ajitahid kwa kweli
David Pere
Huyu jamaa no hatari sana anapoliona kombe uwanjani lazima alibebe
Shafii
Kukosa penati sio kwa Ronaldo tu mchezaji yeyote anaweza kosa penati ninaimani ataparform vizuri
Gabriel
Jambo lilomkuta kwny mech ya ac millan n bahat mbaya
Ester jackson
Cr7 kwa kosa alilolifanya naamini kuwa anaweza kufanya mabadiliko katika timu na hiyo ndiyo storia yake ya kuto shindwa kirahisi
isha
Aongeze juhudi
Elika
Ronaldo anajielewa sana kwanza heshima kwake
Samiah
Aongeze bidiii
Magdalena
Ronaldo ni mahili katika mpira ila anajisikia sana
Omary lukumbi
Cr7 mnyama akuna asiye mjua ila bado uwez upo maana si mtu wa kumbeza maana bado ana uwezo mkubwa wa kufanya makubwa zaid
Tahiya
Cristian Ronaldo ni mchezaji mzuri anajituma mno na anajua nini afanye hawapo uwanjani kilichotokea kwnye mechi ya nusu fainali ni bahati mbaya tyuu kukosa penati
Mwanaidi
Kujikwaa sio kuanguaka naamini atafanya vizuri kwani ukiongelea wachezaji bora lazima umtaje huyu mnyama CR7 amefanya maajabu mengi makubwa kwenye huu limwengu wa soka tusubirie tuone atakavyopiga tiktaka
Khadija
Ronaldo ni mxhezaji ninayemkibali sana #meridianbettz
Khadija
Ronaldo ni mxhezaji ninayemkunali sana#meridianbettz
Adelta
Ronald anajitambua Sana namkubali
warda
Namwaminia CR7 atafanya maajabu#Meridianbettz
Neema hassan
Mchezaji mahiri
Hope mwaikuka
Inawezekana tu
Emmy cleopa
Ronaldo anaweza
Devotha
Ronaldo ni mchezaji mzuri atafanya timu yake iibuke na ushindi kwenye fainal inawezekana
felister
Ronaldo mtu mbaya
Caroline
Ronaldo mbona Leo yupo vizuri jmn.
lombo
CR7 namkubali sana hawez rudia kosa
Salma
Uwenda umri ukamtupa mkono
Njiku
Cr7 hupo poa sana
Dorophina
Ronaldo yupo vizuri naamini atafanikiwa tu
Hamidu
CR7 mnyama leo anarekebisha makosa yake#meridianabettz
Ernest
Ukimuangalia CR7 ni mchezaji anaayeweza kucheka na nyavu kwa wastani wa kila mechi
Genia Sikaluzwe
Ronald ni mchezaji mahili Sana wa mpira
Sadick
Mechi ya kwanza baada ya miezi 3 nje wachezaji bado hawajafanya mazoezi ya kutosha. Hope CR7 atafanya vizuri mechi ijayo#meridianbettz
Sabrina
Maoni:Cr7 anajitambu,yuko vzuri
Furahav
Anajua CR7
Zeiyana
Cr 7 naamini harudiagi makosa atafanya vizuri
Amani
CR7 atafanya maajabu#Meridianbettz
Tatu
Cr7yupo vizuri