Beki wa Real Betis Luiz Felipe amefikia rekodi ambayo bado haijawekwa baada ya kutimuliwa uwanjani hapo jana kwenye mchezo wao waliokuwa wanacheza dhidi ya Celta Vigo.

Kutolewa kwake katika dakika ya 95 katika mechi ya jana waliyochapwa 4-3 na Celta Vigo ilikuwa kadi yake nyekundu ya tatu msimu huu katika mechi 11 pekee za ligi.
Felipe alishiriki katika mechi mbili pekee kati ya saba zilizofuata za Betis kwenye LaLiga, kabla ya kufukuzwa kwa mara ya pili msimu huu dhidi ya Athletic Bilbao mnamo Desemba 29.
Akiwa nje ya kikosi kwa karibu mwezi mmoja kabla ya kurejea Januari dhidi ya Getafe, Felipe alihifadhi nafasi yake kwa mechi iliyofuata dhidi ya Barcelona na pambano la jana dhidi ya Celta Vigo.

Lakini, kadi nyekundu ya tatu ya kampeni katika mchezo huo inampa Felipe rekodi ya kipekee ya kinidhamu, baada ya kupewa kadi nyekundu katika mechi mbili kati ya nne za mwisho na mara tatu katika saba zilizopita.

