Laporta: Messi ni Mchezaji Bora wa Muda Wote

Rais wa klabu ya Fc Barcelona Joan Laporta amesema kua mchezaji wa zamani wa klabu hiyo ambaye kwasasa anacheza klabu ya PSG Lionel Messi ndio mchezaji bora wa muda wote.

Mchezaji Lionel Messi amefanikiwa kushinda taji la kombe la dunia siku ya jumapili wakiifunga timu ya taifa ya Ufaransa katika mchezo wa fainali, Taji pekee ambalo mchezaji huyo alikua amelibakisha kwenye maisha yake ya soka.laportaKufuatia kushinda taji la kombe la dunia kwa mchezaji Lionel Messi kumeibua mijadala mbalimbali wengi wakihitimisha kwa kusema kua ndio mchezaji bora wa muda wote kuwahi kutokea, Na Rais Laporta nae ameungana na wadau wengine akisema mchezaji huyo ndio mchezaji bora wa muda wote.

Rais huyo wakati akifanya mahojiano na waandishi amempongeza mchezaji huyo wa zamani wa klabu yake na kusema mchezaji huyo ni shabiki mkubwa wa klabu hiyo  na pia mapigo yake ya moyo yanadunda Barcelona.laportaRais Laporta alipoulizwa kuhusu kumrudisha mchezaji huyo klabuni hapo “Ni mchezaji wa klabu ya PSG kwasasa, Lakini siku tutamrudisha Messi hapa” Kutokana na kauli ya Rais huyo inaonesha moja kwa moja klabu hiyo ina mpango wa kumrudisha mchezaji huyo ndani ya Barcelona siku moja.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.