Ushangiliaji Mpya Unamponza Ronaldo!

Mshambuliaji wa Juventus, Cristano Ronaldo anaripotiwa kuwa chini ya uchunguzi kufuatia ushangiliaji wake mpya kwenye gemu dhidi ya Atletico Madrid ambayo alichapa magoli matatu na kuisaidia klabu yake kuingia hatua ya robo fainali.

Ronaldo alikuwa shujaa wa alikuwa Shujaa wa Juventus, baada ya kuondoa gepu la 2-0 la kwenye mzunguko wa kwanza kwenye hatua ya mtoano wa klabu 16, Magoli yake matatu yalikuwa ni kila kitu walichokihitaji Juve kuingia robo fainali.

Goli la tatu la staa huyu lilipatikana kwa mkwaju wa penati, na baada ya kuchapa goli hilo alikimbia na kushangilia tufauti na anavyoshangilia wakati wote, hapa aliongeza mbwembwe na alishangilia mbele ya mashabiki wa Atletico akimuiga Diego Simione alivyoshangilia kwenye gemu ya kwanza. Hata hivyo staili aliyoitumia staa huyu inatafsiriwa kuwa kama aliwatukana mashabiki wa Atletico.

Ushangiliaji Mpya Unamponza Ronaldo!
Ronaldo akishangili

Taarifa zianadai UEFA wanafanya uchunguzi kufuatia aina hiyo ya ushangiliaji. Huenda staa huyu akakutana na adhabu. Inahofiwa kuwa huenda akakosa gemu moja au zote 2 za robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya au akalipishwa tu faini inategemea na maamuzi yatakayotolewa.

Diego Simione, meneja wa Atletico ambaye alishangilia hivyo kwa mara ya kwanza alikutana na rungu la UEFA na kutakiwa kulipa faini ya paundi 20,000, hivyo huenda Ronaldo akapewa adhabu sawa na hiyo.

3 Komentara

    Gud news

    Jibu

    Good news 👍

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.