Kuelekea muendelezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara [VPL], baadhi ya timu zilizokuwa na michezo pungufu kuanza safari yao mapema.
Simba SC na Namungo zinamichezo pungufu, hii ni kutokana na ushiriki wa timu hizi kwenye mashindano ya Caf Champions League sambamba na Caf Confederation Cup.
Taarifa rasmi kutoka bodi ya Ligi [TPLB], imetangaza tarehe ambazo timu hizi zitacheza baadhi ya michezo yao waliyonayo mikononi.
Februari 4, Simba SC watachuana na Dodoma Jiji katika dimba la Jamhuri, Dodoma. Siku hiyo hiyo, Namungo watapambana na KMC FC katika uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam.
Februari 7, Namungo watawakaribisha Ruvu Shooting FC pale Majaliwa Stadium. Wakati huohuo, mabingwa watetezi wa VPL – Simba SC watapambana uso kwa uso na Azam FC katika uwanja wa Benjamin William Mkapa.
“Mechi zilizosalia ikijumuisha Namungo dhidi ya Gwambina na Simba SC dhidi ya Namungo, zitatolewa taarifa baadae.” iliripoti bodi ya Ligi [TPLB].
Anayejaribu hawezi kutoka kapa Meridianbet! Kasino ya mtandaoni ya Meridianbet inakuhakikishia ushindi mkubwa kila unapojaribu kuingia mchezoni. Washindi hushindana, ingia mchezoni!



Magdalena
Afadhali tulikuwa tunasubiri kwa hamu
Adelta
Mashabiki tunasubiri tuone
Khadija
Mashabiki tunasubili kwa hamu
Caroline
Yetu macho
Sania
Mashabiki tunasubiri kwa hamu
Sarah
Tunasubiri tuone
Mwanahamisi
Ngoja tuone
Dorophina
Mechi itakuwa na ushindani mkubwa
Zahara Omary
Ngoja tuone
Lydia Emmanuel Magoti
Tunasubili tuone
Hopemwaikuka
Fresh
Rahmal
Nice
samiah
Safi
warda
Azam wametuaribia pozi