Chelsea Bado Inamuhitaji Wilian

Willian Borges da Silva kwa kawaida anajulikana kama Willian alizaliwa tarehe 9 Agosti 1988 ni mchezaji wa soka wa Brazil ambaye anacheza kama kiungo mshambuliaji katika klabu ya Chelsea na timu ya taifa ya Brazil. Willian alianza kucheza katika timu ya Brazil mwaka 2011 na aliliwakilisha taifa lake katika Kombe la Dunia la FIFA ya 2014, Copa America ya 2015 na Copa America Centenario.

Willian akishangilia Goli aliloshinda akiwa na Brazil

Mnamo tarehe 31 Januari 2013, Willian alihamia Anzhi Makhachkala. Awali alichagua kuvaa namba 10, hata hivyo kutokana na vikwazo vya UEFA ambavyo inasema mchezaji lazima avae nambari inayotumiwa katika Ligi ya Mabingwa, alilazimika kuvaa namba 88 aliyoichagua akiwa Shakhtar.

Baada ya kuhamia Urusi, Willian alisema alifurahi kujiunga na Anzhi na aliitakia Shakhtar Donetsk mafanikio makubwa katika siku zijazo. Kwa mara ya kwanza, Willian alishambulia Newcastle United katika Ligi ya Europa.Pia alifunga bao lake la Anzhi pekee mnamo 14 Aprili 2013 katika ushindi wa 3-0 dhidi ya Volga Nizhny Novgorod.

Mnamo tarehe 25 Agosti 2013, klabu ya Uingereza ya Ligi Kuu ya Chelsea ilikubali kusainiwa kwa Willian. Mpango huo ulifanyika rasmi tarehe 28 Agosti 2013 na Willian alijiunga kwa mkataba wa miaka mitano, akipokea shati namba 22 mgongoni.

Willian alianza kucheza rasmi katika klabu ya Chelsea mnamo tarehe 18 Septemba dhidi ya Basel katika Ligi ya Mabingwa. Baada ya kushinda dhidi ya Swindon Town na Steaua Bucureşti katika Kombe la Ligi ya Mabingwa,Chelsea ilicheza mechi dhidi ya Norwich City mnamo terehe 6 Oktoba na kushinda 3-1.Pia aliisaidia Chelsea kushinda 2-0 dhidi ya Liverpool.

Magoli mawili ya mwisho kabla ya zuio la lazima la kuahirisha msimu wa mwaka 2019/20 katika ligi kuu ua Uingekleza yalifungwa ama kusababishwa na Wilian.

Kutokana na uwezo mkubwa wa Wilian kuna uwezekano  mkubwa wa kocha mkuu wa timu ya Chelsea Frank Lampard kumuongeza mkataba Mpya mshamuliaji huyo ili aendelee kubaki Darajani, Ingawa Lampard ana mikakati ya kukuza Zaidi farsafa ya mpira wa vijana bado Wilian mwenye miaka 31 kwa sasa anaweza kubaki na Chelsea.

4 Komentara

    Vizur

    Jibu

    Kabisa bado tunamuhitaji

    Jibu

    Gud news

    Jibu

    Ni moto tu utawaka

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.