Gareth Bale anajiandaa kuwa mchezaji wa pili kwenye timu ya taifa ya Wales kufikisha michezo 100, ikiwa atacheza kwenye mchezo wa kufuzu kombe la Dunia 2022 dhidi ya timu ya taifa ya Belarus.
Gareth Bale ambaye amekuwa nj’e ya uwanja kwa takribani miezi miwili baada ya kupata majeraha ya misuli ya paja, lakini kwasasa anajiandaa kuiongoza timu ya Wales kwenye mchezo wake wa mwisho wa kufuzu kombe la Dunia 2022, kwenye jiji la Cardiff siku ya jumamosi.

“Kufikisha michezo 100 mimi kwangu ni mafanikio makubwa, huwezi kufikilia kwa mara ya kwanza, lakini unapokuwepo kwenye hicho kilele ni jambo zuri kwangu na kwa familia na natumai watafurahia.” alisema Bale
Bale hakuichezea timu ya taifa ya Wales tokea tarehe 8 septemba kwenye mchezo dhidi Estonia ulioisha kwa sare ya bila bila.

“Sikua kwenye kiwango kizuri kama nilichokuwa nacho kabla ya majeruhi. Nimejitahidi kwa juhudi zaidi ya nilivyojaribu na nimerudi.”
“Sina hakika kama nitacheza mechi nzima, nina wasiwasi kwa sababu sikucheza kwa miezi miwili, lakini nitajitoa kwa silimia 100 na hivyo ndivyo nilivyojihakikishia.” aliongezea Bale.

Chris Gunter ndiye anyeshika nafasi ya kwanza kucheza michezo mingi kwenye timu ya taifa ya Wales, huku akiwa amecheza michezo 106.
Unawezaje kuikosa hii! njia rahisi ya kutengeneza mkwanja katika kasino maridhawa za meridianbet. Muda wa kufurahia na kutengeneza mkwanja ipo mikononi mwako unasubiri nini?


