Bingwa mtetezi wa michuano ya Tenis ya Australian Open Caroline Wozniacki ametoboa kuingia kwenye raundi ya tatu kwa ushindi wa moja kwa moja dhidi ya Johanna Larsson. Sasa atamvaa Sharapova!
Bingwa huyu alitumia mda wa dakika 66, saa 1 na dakika sita kumchapa mpinzani wake anayetajwa kuwa nafasi ya 75 ya viwango vya mchezo huu. Amemchapa kwa seti ya 6-2 6-1.

Wozniacki atamvaa Sharapova
Ushindi huu unampeleka Wozniacki kwenye raundi ya 3 kupambana na Maria Sharapova bingwa aliyeshinda michuano hii mwaka 2008. Sharapova ambaye pia ni bingwa mara 5 wa Grand Slam alimtandika Rebecca Peterson wa Swideni kwa seti ya 6-2 6-1.
Pia, kwenye michuano hii mwanadada bingwa wa mara 3 wa Grand Slam, Angelique Kerber alimchapa Beatriz Haddad Maia 6-2 6-3.


Fatina
Taarifa nzur meridian
Furahav
Carolina yuko vizuri sana.
Povel
Corona noma