Masuala ya kodi imekuwa ni tatizo kubwa sana huko majuu Hispania ikihusisha wasakata kabumbu na makocha!
Siku kadhaa nyuma waendesha mashtaka wa nchini huko wametaka mchezaji wa zamani wa klabu za Liverpool, Bayern Munich na Real Madrid, Xabi Alonso afungwe jela!
Kwa sasa mchezaji huyo amestaafu na kifungo chake kinaweza kuwa ni kwa muda wa miaka nane na nusu akituhumiwa kuwa na kosa la kutumia udanganyifu kwenye malipo ya kodi akiwa huko.


Sadick
Nadhani Spain kuna mianya mingi ya wanasoka kukwepa kodi maana imekuwa ni kawaida kwa visa hivi kutokea mara kwa mara, ilikuwa hivyohivyo kwa Mourinho, Ronaldo na Messi#meridianbettz
Povel
Habar njema
Issa
Apewe adhabu kali maana vitendo hivi vimekithiri