Kocha wa Klabu ya Manchester City Pep Guardiola amewaonya wachezaji wa klabu yake kua wasitarajie faragha baada ya kufanya vitendo ambavyo sio vya kinidhamu na hiyo imekuja baada ya kitendo cha beki wa klabu hiyo Kyle Walker.
Pep Guardiola amezungumza baada ya beki wa klabu yake Kyle Walker kunaswa na kamera akiwa baa moja jijini Manchester akionekana kushusha suruali yake, Kutokana na kitendo hicho kilifanya mchezaji huyo kukamata kichwa cha habari kwenye magazeti mbalimbali ya nchini Uingereza.
Kupitia Kitendo cha Kyle Walker kilifanya kocha huyo kuwaonya wachezaji wake kutokurudia kitendo cha alichofanya mchezaji mwenzao Kyle Walker, Kocha huyo hategemei kuona kitendo hicho kinatokea kwa wachezaji wengine ndani ya kikosi cha Manchester City.
Kocha Guardiola wakati akizungumza na wanahabari na kuzungumzia kitendo cha beki wake Kyle Walker kocha huyo alisema kua kitendo ambacho amekifanya beki wake ni cha faragha, Lakini akisema wataongea na mchezaji huyo faragha ili kuhakikisha kila kitu kinakaa sawa.
Kocha Guardiola amezungumza pia kuhusiana na wachezaji kua waangalifu wakiwa nje ya kiwanja, Kocha huyo amesema kua siku hizi mambo yamebadilika akisema wanatakiwa kuwa waangalifu kwasababu wanapaswa kujua sehemu yeyote wanayokuwepo kwasasa wanaweza kurekodiwa.

