Beki kisiki wa Klabu ya Simba, Joash Onyango amesema kuwa yupo vizuri baada ya kupata maumivu kwenye mchezo wao dhidi ya Al Merrikh.
Jana Machi 16 wakati ubao ukisoma Simba 3-0 Al Merrikh, Onyango alipata maumivu dakika ya 43 na nafasi yake ikichukuliwa na Erasto Nyoni.

Ulikuwa ni mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika hatua ya makundi ambapo Simba iliweza kusepa na pointi tatu jumla.
Hali yake ilionekana kuwatisha mashabiki kwa kuwa alitolewa akiwa amebebwa kwenye machela baada ya mpira kumgonga kichwani kwenye harakati za kutimiza majukumu yake.
Onyango amesema:-“Nipo salama na ninaendelea vizuri, nilipata maumivu wakati ule na kuweza kupewa huduma ya kwanza, natarajia kuelekea Kenya kwa timu ya Taifa,”.

Onyango amekuwa kwenye kiwango ndani ya kikosi cha Simba kinachonolewa na Didier Gomes kwa kuwa na maelewano mazuri na Pascal Wawa.
Maana Kamili ya Ushindi Katika Kasino za Meridianbeti ni Pamoja na Mchezo wa Tropical Wild.
Hii ndiyo burudani yenye ushindi! Ingia kwenye kasino ya Meridianbet kufukuzia ushindi huu. Cheza sasa Tropical Wild na uwe moja ya washindi na Mabingwa.



Adelta
Kila la kheri uko uendapo
Lydia Emmanuel Magoti
Duuh pole yake honyango
Hopemwaikuka
Pole sana Josh
Sarah
Pole yake
Caroline
Ni vizuri
Dorophina
Habari njema
Neema juma
Polee yake
Venerose
Kazi popote
Mwanahamisi
Pole yake
warda
Onyango namkubali sana