Kai Havertz kutoka kuwa ‘garasa’ usemi ambao kwa Tanzania ni maarufu wakiwa na maana mchezaji asiyekuwa na thamani ‘hovyo’ kulingana na mkwanja uliotumika kumsajili hadi kuwa shujaa chini ya Thomas Tuchel ambaye ameonekana kumrejesha Mjerumani mwenzake kwenye makali yake na mwishowe kufunga bao muhimu dhidi ya Manchester City.
Tabasamu lilionekana usoni mwa nyota wa Kijerumani, Kai Havertz anayeichezea Chelsea pale alipoulizwa kuhusu msimu wa 2020/21 ulivyokuwa kwa upande wake mara baada ya kumalizika kwa mchezo wa fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Manchester City.
“Kiukweli sijali. Jambo muhimu tumetwaa Ligi ya Mabingwa Ulaya, “ alisema Kai ambaye bao alilofunga kwenye mchezo huo liliipa ubingwa timu hiyo.
Awali akiwa chini ya Frank Lampard, Kai ambaye ni mmoja kati ya wachezaji wenye thamani kubwa zaidi (Pauni 89 milioni), alionekana kuchemka ikiwa ni kipindi kifupi tangu ajiunge na matajiri hao wa London akitokea Bayer Leverkusen ya Ujerumani.
MAANA KAMILI YA USHINDI KATIKA KASINO ZA MERIDIANBETI NI PAMOJA NA MCHEZO WA PANDA PANDA.
Hii ndiyo burudani yenye ushindi! Ingia kwenye kasino ya Meridianbet kufukuzia ushindi huu. Cheza sasa Panda Panda na uwe moja ya washindi na Mabingwa.
Good
Vizuri
Kai anajitahidi sana
Nice