Kichapo Cha Aibu, Satien Afungashe Virago?

Baada ya Barcelona ya Messi kupokea kichapo cha aibu cha goli 8 kwa mara ya kwanza tangu mwaka 1946, Quique Satien na Barcelona bila shaka wanaenda kupeana talaka.

Satien, ambaye kikosi chake kimepokea kichapo cha 8-2 dhidi ya Bayern Munich, amesema kuwa Barcelona wanahitaji kurejesha heshima yao baada ya kuruhusu kichapo hicho kwenye Ligi ya Mabingwa.

Lakini ripoti zinasema kuwa meneja huyu, yuko mbioni kutimuliwa baada ya kile kilichotokea. Unafikiri ni wakati wake wa kufungasha vilago?

Kipindi cha kwanza pekee, kilitosha kuwavujisha jasho Barcelona wakienda mapumziko tayari wakiwa wamekubali bao 4-1, na goli 1 Bayern wakiwa wamejifunga. Ikumbukwe walikuwa wanaingia mechi hii wakiwa na hasira na majuto ya kuvuliwa ubingwa wa LaLiga na Real Madrid.

Mlinzi wa Barcelona, Gerard Pique ametoa wito kwa klabu kufanya mabadiliko katika nyanja zote za kikosi, unafikiri amegusia pia kuenguliwa kwa Meneja? 🤔

Satien, ambaye ambaye alichukua kibarua cha umeneja mikononi mwa Ernesto Valverde mwezi Januari amesema kuwa “Pique ni mchezaji ambaye amekuwepo hapa karibu maisha yake yote ya soka, mimi nimekuwepo hapa kwa miezi sita au nane, alichokiongea kinaingia akilini lakini mimi sio mtu sahihi wa kuliongelea hilo.”

Kichapo hiki kimewaumiza mashabiki wa Barcelona, maumivu haya yatachukua mda kupotea, lakini kibarua cha Satien kipo mashakani kwa sasa.


 

Umekuwa mteja muaminifu wa meridianbet? Kuna zawadi kibao hadi 5% ya pesa yako inarejeshwa kwako. Kila wiki unaweza kurudishiwa mpaka Tsh 250,000.

soma zaidi

39 Komentara

    Asante kwa taarifa

    Jibu

    Duuh pole sana kocha wa barcelona maana hicho sio kichapo kidogo kibongo bongo tunaita kichapo cha mbwa

    Jibu

    Hii habari mbaya Barcelona ya zamani sio ya sasa sio kwa kichapo kile anatakiwa kocha angalie wakae chini wajipange upya wakizubaa kichapo kile kile kitawafuata

    Jibu

    Kweli Maisha yanaenda kasi sana Barc wa kufugwa goli nane kweli?ha haaaaaaaa#Meridianbettz

    Jibu

    Duh pole Sana kocha wa Barcelona
    @meridiabettz

    Jibu

    Kwa kweli ni aibu dahhh

    Jibu

    Barca wameanza kutepeta sio kwa kichapo kile cha jana na Messi akiwepo ndani Barca na Messi wake saiz amna kitu

    Jibu

    Ni habari mbaya sana Barcelona ya zaman sio ya sasa sio kwa kichapo kile#Meridianbettz

    Jibu

    Kazi anayo kocha

    Jibu

    Hii ilikua aibu kubwa sana kwa klabu kama Barcelona kutandikwa goli nane kwa mechi moja yani bora ingekua labda kuna home and away achapwe 4 alafu tena nne ila 8 kwa wakati mmoja duu,ina maana kungekuwa na home and away angechapwa magoli 16?Aibu sana hii lakini nayo inanikumbusha kipindi kile Arseanal alifungwa bila huruma goli 8 na Manchester Utd ila wao hawakufukuza kocha.Kocha wa Barcelona keshafukuzwa toka jana na ni muda muafaka sasa wa klabu kusukwa upya kwani enzi zakina Pique,Mesi zimeshaisha sasa..

    Jibu

    Daaah kama mpira wa mikono

    Jibu

    Sio tu Satien ila wachezaji wengi, Aksante kwa Countinho kwa kutunyoosha kisawasawa

    Jibu

    Quique Satien should go#meridianbettz

    Jibu

    Duu noma Sana Barcelona walicho kifanya Jana haibu kumfukuza kocha Satien sio ndio timu itakaa sawa akuna nimwelekeo wao aukukaa sawa huwanjani nivitu vyakukaa nakuongea kupanga tumekosea wapi namakosa yalekebishwe

    Jibu

    kweli zama zimebadilika

    Jibu

    Kwa matokeo hayo hata Mimi ningekua bosi ningekimbiza tu.

    Jibu

    Haibu kubwa kwa kweli clabu kubwa kama Barcelona kuchapwa magoli mengi kama vile mpila wa kikapu khaaa..!wamewashinda hata yanga

    Jibu

    Afungashe tu virago aende Barcelona ni timu kubwa kwa kutoa matokeo ya jana ni fedheha kubwa timu

    Jibu

    Duuu inahuzunishaaa kweli poleni Barcelona

    Jibu

    Dah kazi ipo jmn cocha

    Jibu

    Barcelona jana walipoteana mapema sana hivyo kuwapa Bayern Munich uwaz mapema ila Kama wangejipanga mapema ile gem wangeweza kukabiliana nao kabisa kiukwel walionyesha udhaifu kwny mabek wa Kati na mbele kulikuwa vbaya kabisa

    Jibu

    Barua inakuusu kocha sio kwa aibu hiyo

    Jibu

    Asante kwa makala

    Jibu

    Satien kubaki ni asilimia ndogo sana kwa kipigo cha jana kocha ndio atawajibishwa lakin ni wachezaji wenywe walipotea vibaya walizidiwa maarifa na bayern

    Jibu

    Open door SATIen let go,🏃🏃🏃🏃🏃🏃

    Jibu

    Barcelona wameshinda sana sasaivi pia na mabeki hawana

    Jibu

    Kazi ya ukocha ugumu wake upo hapoo anatakiwa afungashe kilicho chake akwende

    Jibu

    Daah ila ndo mpira hulvyo.

    Jibu

    Hata m nisingeweza kwakwel ni aibu sana

    Jibu

    Daah! Ila Bayern wanasifa Sana hiyo ni komoa

    Jibu

    Tunao umia ni sisi mashabiki

    Jibu

    Hayo ndio maisha ukocha ukiwa kibaruan

    Jibu

    Barcelona wanatakiwa waongeze bidii katika mazoezi

    Jibu

    Kwa matokeo haya sidhani kama Luna viongozi watakao endelea

    Jibu

    Kiukwel afanye aende tuu,maana ni aibu sana!!

    Jibu

    Hii ilikua aibu kubwa sana kwa klabu kama Barcelona kutandikwa goli nane kwa mechi moja yani bora ingekua labda kuna home and away achapwe 4 alafu tena nne ila 8 kwa wakati mmoja duu,ina maana kungekuwa na home and away angechapwa magoli 16?Aibu sana hii lakini nayo inanikumbusha kipindi kile Arseanal alifungwa bila huruma goli 8 na Manchester Utd ila wao hawakufukuza kocha.Kocha wa Barcelona keshafukuzwa toka jana na ni muda muafaka sasa wa klabu kusukwa upya kwani enzi zakina Pique,Mesi zimeshaisha sasa.kilichobakia kwao waende MSL tu

    Jibu

    barcelona kwa kichapo walichokipokea cha aibu sana yani wangepangua wachezaji wote na kukisuka upya kikosi icho ili wasijepokea tena aibu ya aina iyo

    Jibu

    Kweli kabisa imekua na matokeo mabovu mnoo

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.