Toto Wolff ataamua hatma yake kuhusu kusalia kwenye uongozi wa timu ya Mercedes kunako michuano ya Formula One – F1.
Chini ya uongozi wa Wolff, Mercedes imekuwa timu yenye mafanikio makubwa katika historia ya Mashindano ya F1 lakini mkataba wake unaisha mwishoni mwa mwaka huu. Wolff amesema anajadiliana na mkurugenzi mkuu wa Mercedes – Ola Kallenius.

“Ninasababu nyingi za kutaka kubaki, lakini ni mchakato. Hakuna sababu ya kutokuendelea kuwepo. Tutajua ni katika nafasi ipi.”
Wolff anamiliki 30% ya hisa za Mercedes na ni kiongozi wa timu hiyo. Wolff amenukuliwa akisema, ” tunataka kufanya vizuri kwa kila kinachowezekana na kuiona timu yetu ikisonga mbele. Ninaifurahia nafasi yangu na mipango yangu ni kuendelea kuongoza, lakini sitaki kuwa kwenye hali ya kushuka kutoka kwenye ubora mkubwa na kuwa na ubora wa kawaida.”
Dereva wa Mercedes – Lewis Hamilton amesema anahitaji ufafanuzi kuhusu hatma ya Toto Wolff kabla hajaingia makubaliano mapya na timu hiyo. Japokuwa, Wolff haamini kama hatma yake inamatokeo yeyote kwa Hamilton.

Wolff anasema ” Kubaki kwa Lewis ni kitu kikubwa sana na yeye binafsi anataka kubaki. Ana nafasi ya kushinda vitu vingi zaidi, inahamasisha kusikia kwamba kubaki kwake kutategemea maamuzi yangu lakini hanihitaji mimi.”
“Bado sijafanya maamuzi, haya ni majadiliano yanayoendelea kwa sasa na yanamuelekeo chanya, ninayafurahia. Sitaki kuwagusia kwamba ninaondoka kwa sababu sio kweli. Nipo kwenye wakati wa kutafakari muelekeo wa F1, kinachotokea baada ya Corona na sababu zangu binafsi.”
Wolff pia amegusia kwamba kunamazungumzo yanayoendelea kati ya Mercedes na F1 kuhusu mkataba mpya utakao wapa nafasi Mercedes kushiriki michuano hiyo baada ya mwaka huu.

“Wiki iliyopita nilikuwa nina mazunguzo mazuri na Mkurugenzi wa F1 – Chase Carey. Vitu vingi tulivyohitaji ufafanuzi vimefanyiwa kazi na ninadhani tupo kwenye nafasi nzuri ya kusaini mkataba wa ‘Concorde Agreement’. ”
Mkataba wa Concorde Agreement ni msamiati unaotumika na F1 kwenye mikataba kati ya timu shiriki na F1 ambayo [mikataba] ilianzishwa 1981.
Umekuwa mteja muaminifu wa meridianbet? Kuna zawadi kibao hadi 5% ya pesa yako inarejeshwa kwako. Kila wiki unaweza kurudishiwa mpaka Tsh 250,000.


neema hassan
Asante kwa taarifa#meridianbettz
Omary lukumbi
Asante kwa taarifa
Issa
Itakua pigo kwa mercedes team
Gabriel
Hatar sana
Hope mwaikuka
Duh!
David Pere
Toto Wolff ataamua hatma yake kuhusu kusalia kwenye uongozi wa timu ya Mercedes kunako michuano ya Formula One – F1 Kama ataona umuhimu wake
Mwanahamisi
Hatari sana
aisha
Mercedes wamepata pigo kubwa sana
Tatu
Wolff awezi kuondoka hapo anamiliki hisa ya 30%mercedes na ni kiongozi wa timu hiyo
Nasra
Duh Sio poa hii
Lydia Emmanuel Magoti
Duu noma sana
Sadick
Toto Wolf ni jina kubwa ndani ya formula one baada ya mwanzilishi wake Bernie Ecclestone#meridianbettz
felister
🔥
Furahav
Baki tu
Venerose
Mmmh
Sabrina
Duh hatari
Samiah
Duuh hatari
farida ahmadi
Ni maamuzi yake binafsi
magdalena
wolff afanye maamuzi mengine lakini kuondoka apo sio kazi rahisi kwake kutokana na hisa alizokuwa nazo
Magdalena
maamuzi yake ni sahihi kwake
Amiri Kayera
Yah good
Neema
Duu noma sana