Kocha wa klabu ya Liverpool Jurgen Klopp ametaka mchezo wao uliopigwa wiiendi iliyomalizika dhidi ya klabu ya Totenham Hotspurs kurudiwa kutokana na makosa yaliyofanywa na waamuzi.
Kocha Klopp anaona kua fidia ambayo itawafaa ni kurudia mchezo wao dhidi ya klabu ya Tottenham, Lakini tofauti na hapo sio jambo ambalo watakua wameridhishwa nalo kabisa.
Klabu ya Liverpool iliombwa radhi na chama cha marefa wa ligi kuu nchini Uingereza na hiyo ni baada ya kukatiliwa bao lao katika mchezo dhidi ya Tottenham lililofungwa na Luiz Diaz, Ambapo ilikuja kufahamika bao hilo lilikua halali na mchezaji hakuotea kama ambavyo ilitafsiriwa awali.
Kumekua na mvutano baada ya mchezo huo kwani mchezo huo pia ulikua na maamuzi ya kustaajabisha, Kwani klabu ya Liverpool ilipata kadi nyekundu mbili ambapo moja ya kadi hizo pia klabu hiyo wamelalamikia na kutaka kukata rufaa kwa madai haikua halali.
Baada ya chama cha marefa ligi kuu ya Uingereza kuiomba radhi klabu ya Liverpool kutokana na makosa yaliyofanyika katika mchezo wao ambayo waliyaita makosa ya kibinadamu, Lakini kocha Jurgen Klopp anaona fidia sahihi na itakayowaridhidha ni kurudia mchezo japo yeye mwenyewe anaona ni ngumu kutokea.

