Lampard Kuelekea Chelsea vs Crystal Palace

Mkutano wa kocha Frank Lampard hii leo kabla ya mechi ya kesho ambapo Chelsea itakuwa ugenini kuikabili Crystal Palace.

“Kante hatokuwepo kwenye kikosi kutokana na majeraha ya nyama za paja. Kovacic amefanya mazoezi ingawa ataukosa mchezo pamoja na Tomori nategemea anaweza kurejea wiki ijayo.”

Kama ushindi wa jumamosi umeirudisha Chelsea kwenye njia;
“Sidhani kama tulikuwa nje ya njia. Kila mechi ni ngumu. Crystal ni timu ngumu pia iliyojipanga zaidi kwenye kuzuia hivyo tunatakiwa kuchagua njia sahihi ya kuukabili mchezo.”

Kama Man utd ni mpinzani mkubwa kwa Chelsea;
“Ni mpinzani mkubwa kutokana na aina ya kikosi walichonacho. Wachezaji wake watatu wa mbele wote wanafunga magoli mengi na wana hali ya juu. Ni wapinzani wakubwa lakini kinachotakiwa zaidi ni jinsi gani utamaliza msimu.”

Kuhusu kurejea kwa Loftus-Cheek na Hudson-Odoi;
“Kwa Loftus-Cheek hiki ni kipindi chake muhimu cha kurejea mchezoni na kujiweka sawa lakini msimu ujao ndicho kipindi atakuwa kwenye ubora zaidi. Lakini hiyo haimaanishi kama kwasasa hawezi kuwa bora.”

 

“Ni hivyo hivyo kwa Callum pia, lakini yeye anatakiwa kuhakikisha anafanya mazoezi kwa bidii sana ili azidi kuwa vizuri. Kwasasa tunaona kile ambacho Pulisic na Willian wanakifanya, basi vile ndivyo anatakiwa kufanya Callum au ata kwa ukaribu wake.”

Kuhusu Jorginho kuziba pengo la Kante;
“Ni mchezaji mzuri. Na anataka sana kucheza na hilo kila mchezaji analitaka. Na mara zote amekuwa akifanya mazoezi vizuri. Kila mchezaji ana umuhimu wake tofauti ipo kwenye uchaguzi wa kikosi tu. Na sitaki kuelezea sababu ya kwanini nimechagua uyu acheze ama yule asicheze. Muhimu zaidi ni kutambua wachezaji wote ni machaguo yangu.”

 

Tofauti ya Eden Hazard na Christian Pulisic;
“Kwakuwa nimewai kucheza na Hazard, namtambua kama mchezaji mwenye kipaji kikubwa ambaye anaweza kuwavuta mabeki wamkabe yeye uku akitengeneza nafasi kwa wengine. Wakati Pulisic ni mchezaji zaidi anayetazama mbele, kitu ambacho nakipenda.”

“Ni aina ya mchezaji akipata mpira atapambana kuhakikisha anavunja mhimili wa mabeki kisha anashambulia. Ukizungumzia kuwalinganisha kwa hapo nitakaa pembeni. Hazard ameshakuwa hapa na amefanya makubwa.”

41 Komentara

    Namkubal sana Lampard

    Jibu

    Mechi itakua bombo sana

    Jibu

    Don’t miss Pulisic & Zaha

    Jibu

    Ni mechi ngumu sana kwa chelsea sababu crystel wana zaha ambae ni msumbufu eneo la penati

    Jibu

    Mechi itakua bombs sana

    Jibu

    Maoni:kukosekana kwa kante itawapa ugumu chelsea kwa kiasi fulan hivi

    Jibu

    Hii si yakukosa

    Jibu

    Itakuwa hatari sana

    Jibu

    Leo patachimbika.

    Jibu

    Lampard ni kocha mzr na anaijua.vzr Chelsea ila atakua na kibarua kizito

    Jibu

    Patachimbika hapo maana wote wanatetea nafasi zao

    Jibu

    Itakua poa

    Jibu

    Siwezi kukosa pesa

    Jibu

    Ni mechi ngumu Sana ila kwa Chelsea wanapaswa kushinda hii mechi kujiakikishia nafasi nzuri ya top 4 ili washiliki club bingwa msimu ujao.

    Jibu

    Cyakukosa hii mechi

    Jibu

    Kibabae sanaa

    Jibu

    Chelsea mpo vizuri

    Jibu

    Itakuwa poa sanaaa

    Jibu

    Mechi ya kibabe.

    Jibu

    Mechi kali

    Jibu

    Wameponea chupu chupu kutoa draw# meridianbettz

    Jibu

    Sawa tu.

    Jibu

    Mechi ilikua kal

    Jibu

    Bora Angekuwepo Kante ila wanaweza kushinda #Meridianbettz

    Jibu

    Hii sio ya kukosa

    Jibu

    Mechi utakuwa ya kibabe

    Jibu

    Mechi ngumu sana ila kwa Chelsea wanatakiwa kushinda kujiweka katika nafasi zaidi nzuri kwao

    Jibu

    Lampard namkubali Sana anajituma na anajua Nini anafanya

    Jibu

    sidhani km Chelsea anaweza shinda iyo mechi

    Jibu

    Mechi ilikuwa inaonyesha lazima Chelsea washinde ili wajiweke sehemu nzuri ya kiwepo nne bora

    Jibu

    Lampard najua ameiandaa vizuri sana timu yake

    Jibu

    Lampard namkubali sana

    Jibu

    Mechi Kali Sana hii siwezi kukosa kabisa

    Jibu

    Chelsea lazima ashinde

    Jibu

    Leo patachimbika

    Jibu

    duuh mpira uwanjani tutaona nani mkali kwa mwezie#meridianbettz

    Jibu

    Lampard ni kocha mzuri sana

    Jibu

    Lampard anakuja vizuri

    Jibu

    Lampard yupo vizuri

    Jibu

    Pulisic ni bonge la mchezaji

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.