Manchester City Waanza Kwa Kupindua Meza

Manchester City walishindwa kutetea ubingwa wao msimu uliopita, wakati Liverpool wakilitia mikononi taji la Ligi Kuu baada ya miaka 30 ya kusubiri. Kibarua walichonacho mkononi kwa sasa ni kurejesha taji walilopoteza msimu uliopita.

Msimu huu umeanza vyema Manchester City pale Molineux baada ya kumuacha mwenyeji wake Wolverhampton kwa kichapo cha bao 1-3.

Mechi hii ilikuwa ngumu kwa wenyeji, huku wageni kimahesabu wakiucheza mpira mwingi na mashambulizi.

Safari ya ushindi ya Man City ilianzishwa na goli la Kevin De Bruyne dakika ya 20 baada ya kuona nyavu kwa penati, kabla ya Phil Phoden hajachungulia nyavu kuongeza goli la pili dakika ya 32.

Paul Jimenez wa Wolves alijaribu kuwafuta machozi kwa goli la kwanza na la mwisho kwa timu yake dakika ya 78, huku Gabriel Jesus akipigilia msumari wa 3 kwa Manchester City.

Inakumbukwa, Wolves alimchapa City nyumbani na ugenini kwa msimu uliopita, bila shaka City hawakupenda kuanza kibarua kwa aibu, na ushindi huu ni mwanzo wa matumaini kuelekea kutetea taji walilolipoteza.

Bila shaka City walijifunza kwa vichapo vya nyumbani na ugenini msimu uliopita na hawakutaka kurudia makosa, washindani wao Liverpool wameshacheza mechi mbili na zote wameandika ushindi.


 

FURAHIA KASINO YA MTANDAONI

Tembelea ardhi ya maajabu ushangazwe na mengi ikiwa ni pamoja na urahisi wa kujipatia utajiri kupitia Kasino ya Meridianbet.

Cheza Sasa

 

35 Komentara

    city wakikazana vya kutosha na juhudi za hali ya juu wanaweza pata ubingwa msimu huu

    Jibu

    Kinachofuata sasa ni kila mtu ashinde mechi zake

    Jibu

    Hapo sasa ndo penyewe

    Jibu

    Man city awakutaka kuludia makosa Yale yale tena kichapo alichokipa nyuma Mfulizo walijipanga vema

    Jibu

    Msimu umeanza vyema kwa man chester

    Jibu

    Man City msimu huu inatakiwa wapambane warudishe taji nyumbani

    Jibu

    Vizuri Sana kinacho fata Sasa kila mechi watoke naushindi wa kupambana

    Jibu

    Ndio walivyo man city wanaazaga vizuri mwisho wasiku akuna kinacho endelea

    Jibu

    Sema hii mechi ulikua ngumu Sana jmn.wamejitaidi mno

    Jibu

    Mancity msimu huu wamekuja kivingine

    Jibu

    Ukiachilia kuwa na wachezaji wazuri pia wana kocha mzuri ambaye ni kocha wa matokeo

    Jibu

    Habarii njema sana hii

    Jibu

    Mancity msimu huu wamekuja kivingine Liverpool wajipange

    Jibu

    Ulikuwa ushindi mno kutoka kwa mpinzani ambae msimu uliopita alifungwa mechi zote#meridianbettz

    Jibu

    Mambo mazuri hayo

    Jibu

    Manchester city wameanza vizur sana 👍

    Jibu

    Manchester msimu huu Kama mtafanya vizuri

    Jibu

    hongera zao bwana

    Jibu

    Nimeona juhudi zao Ila wakaze ndo kwanza kunakucha

    Jibu

    City wakaze tu

    Jibu

    Msimu huu hakuna timu inayotaka kufanya vibaya ila ni mokosa ya mchezaji mmoja mmoja

    Jibu

    City ni kama wamelipiza tu kwa wolves

    Jibu

    saf

    Jibu

    City safari hii wako vizuri sana

    Jibu

    Wameanz na moto

    Jibu

    Wako vizuri sana

    Jibu

    Good news

    Jibu

    Man city wamekuja kwa kasi zaid

    Jibu

    hapo sasa ndo patamu

    Jibu

    Mambo mazuli hayo

    Jibu

    City wakaze buti

    Jibu

    Stil naona city kwa chelsea hatoboi msimu huu

    Jibu

    Mechi ilikua ngumu sana hii

    Jibu

    Kinachofuata sasa ni kila mtu ashinde mechi zake

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.