Mandonga Apiga Mtu Round ya Kwanza kwa T.K.O

Mwanamasumbi ambaye amejipatia umaarufu kwa kipindi kifupi kwenyemchezo wa ngumi baada ya kupoteza mapambano yake mawili yaliofanikiwa kuoneshwa na kutizamwa na wengi nchini Tanzania Karimu Mandonga hatimaye leo amefanikiwa kushinda kwa TKO.

Mandonga kwenye pambano hilo, alikuwa akipigana na Musa Omary. Pambano hilo liliandaliwa na wizara ya sanaa na michezo kwa kushirikiana na BASATA kwa ajiri ya kuhamasisha sensa.

Pambano kati ya Mandonga na Omary lilikuwa sehemu ya kampeni ya serikali ya kuhamasisha wananchi wake kupitia michezo kwa ajiri ya faida ya kuhesabiwa tarehe 23 na wala halikuwa pambano la ushindani.

Mandonga kwenye karenda yake anatarajia kurudi Ulingo mwezi wa tisa ambapo tarehe rasmi bado haijawa wazi ili kurudisha alichopoteza baada ya kupigwa mara mbili mfululizo.

 

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.