Mchezaji wa Manchester United Lisandro Martinez anaamini kuwa klabu yake wako njiani kuwania heshima chini ya Erik ten Hag, lakini anasema United lazima wabaki na msingi kufuatia mabadiliko yao ya msimu huu.

United walianza kampeni kwa kupoteza mfululizo kwa Brighton na Hove Albion na Brentford, lakini wameshinda mechi sita kati ya nane zilizofuata za Ligi ya Uingereza na kushika nafasi ya tano kwenye msimamo.
Kikosi cha Ten Hag sasa kinaweza kupanda hadi nafasi ya nne ambayo kwasasa yupo The Blues hii leo endapo watashinda mchezo wa leo watakapomenyana na Chelsea hadi katika nafasi ya nne bora watakapomenyana na The Blues kwenye Uwanja wa Stamford Bridge Jumamosi, wakiwa wameshinda mechi tatu kati ya nne za mwisho za ligi ugenini.

United ambao wametoka kupata ushindi dhidi ya Spurs wa mabao 2-0, kupitia wachezaji wao Fred na Bruno ndiyo yaliimaliza Tottenham moja kwa moja. Martinez anasema kuwa anafuraha kwasababu walijaribu sana kucheza katika kiwango hicho na wanataka kucheza kwa njia hiyo.
Lakini mchezaji huyo wa zamani wa Ajax alisisitiza umuhimu wa kuwa mtulivu huku akiongeza: “Wakati mwingine tunapaswa kuwa na subira, Hasa mwanzoni, tunajua kwamba hatukucheza jinsi tulivyotaka, “Lakini ni sehemu ya soka, tunajifunza. Ni uzoefu. Tuna timu mpya, mfumo mpya. Sasa inabidi tuendelee.
Martinez pia aliombwa kutaja mfano wake wa safu ya ulinzi, na akachagua Muargentina mwingine mkali, ambaye alishiriki katika ushindi wa taji la Ligi Kuu akiwa na United msimu wa 2006-07.


