Xavi Amzungumzia Frankie Kessie.

Kocha wa klabu ya Fc Barcelona Xavi Hernandez amemzungumzia kiungo wa klabu hiyo Frankie Kessie raia wa Ivory Coast ambaye amesajiliwa klabuni hapo kutoka Ac Milan ya nchini Italia.xaviKocha Xavi amemzungumzia kiungo huyo kutokana na suala la kutokupata nafasi ndani ya klabu hiyo na kufanya baadhi ya watu kuhoji kwani wakati mchezaji huyo anasajiliwa klabuni hapo alionekana ni mchezaji muhimu na ambae anakuja kupata nafasi zaidi klabuni hapo.

“Hapa ni Barca, Hivo ushindani ni mkali. Anafanya mazoezi vizuri sana, Lakini pia ni mtaalamu mkubwa.”Nina uhakika atapata dakika zake ndani ya msimu mzima”Aliesema Xavi wakati anamzungumzia kiungo huyo.

Frankie Kessie ambaye ametoka klabu ya Ac Milan ya nchini Italia ambao ni mabingwa watetezi wa nchi hiyo huku yeye akiwa moja ya wachezaji muhimu zaidi klabuni hapo.xaviLakini Kessie tangu ajiunge na miamba hiyo ya soka nchini Hispania amekua sio mchezaji tegemezi na kutokupata nafasi ndani ya klabu hiyo.

Acha ujumbe