Staa wa Real Madrid, Kylian Mbappé, anaripotiwa kufikia hatua ya mwisho ya uvumilivu wake na idara ya matibabu ya klabu hiyo. Kwa mujibu wa L’Equipe, mchezaji huyo wa Ufaransa amechukua hatua ya kipekee kwa kuwasiliana moja kwa moja na rais wa klabu, Florentino Pérez, akieleza wazi kuwa hataki tena kutibiwa na madaktari wa ndani wa Madrid.

Mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 27 amekuwa akisumbuliwa na jeraha la goti tangu Desemba, lakini inaelezwa kuwa ameridhika kabisa na mbinu za matibabu zinazotumika Valdebebas. Mbappé anataka kufanya kazi moja kwa moja na daktari wake wa zamani wa PSG, Christophe Baudot, ambaye anaamini ndiye aliyemsaidia kurejea kwenye kiwango chake bora hapo awali.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa

Mvutano huo uliongezeka baada ya taarifa kudai kuwa madaktari wa klabu walilenga kutibu mguu usio sahihi mwanzoni. Ingawa Mbappé alijaribu kupunguza uzito wa madai hayo hadharani, hali ya kutokuaminiana inaonekana kuendelea ndani ya kikosi. Inaelezwa kuwa ana hofu afya yake ya muda mrefu inaweza kuathirika kutokana na haraka ya kurejea uwanjani.
Tatizo hili halimuhusu Mbappé pekee. Kiungo Eduardo Camavinga pia alikumbwa na mkanganyiko wa kitabibu, ambapo ripoti zinaeleza kuwa uchunguzi ulifanywa kwenye mguu usio na tatizo, hali iliyochelewesha matibabu sahihi ya jeraha lake la kifundo cha mguu.

Pamoja na drama hiyo, Mbappé kwa sasa yupo na timu ya taifa ya Ufaransa kwa michezo ya kirafiki dhidi ya Brazil na Colombia. Baada ya hapo, anatarajiwa kurejea Madrid kujiandaa na mechi ya La Liga dhidi ya Mallorca, huku Real Madrid wakiwa nyuma kwa alama nne dhidi ya vinara FC Barcelona katika mbio za ubingwa.

