Miongoni mwa ligi zilizochelewa sana kuisha basi ni ligi ya Tanzania bara VPL, lakini bingwa wa ligi hiyo ameshajulikana na hata zile timu zitakazowakilisha taifa kwenye michuano ya kimataifa zimeshajulikana pia.
Siku ya kesho itakuwa siku ya mwisho ya msimu wa 2020/2021, huku viwanja nane vikiwa na mechi 8 tofauti ila zote zikichezwa majira ya saa 10 jioni.
Macho ya watu wengi katika mechi hizi za VPL zitakuwa kwenye ile kati ya Simba na Namungo, ambapo Simba wameahidi mchezo mzuri wa kufurahia ubingwa wao na Namungo wanataka kuharibu sherehe hiyo.

Upande mwingine utakuwa ni kwenye mbio za kusalia VPL msimu ujao, KT Tanzania wanalazimika kushinda ili angalau kuwania nafasi ya ‘play off’ huku wakiiombea mabaya Coastal Union, lakini Mtibwa Sugar nao wanahitaji angalau alama moja muhimu ili kujihakikishia nafasi ya ‘play-off’ huku nao wakiiombea mabaya Coastal Union.
Je, nani atafanikiwa kufanya maajabu kwa siku ya kesho?
Ndio, kama bado hujajiunga na Familia ya Mabingwa ya Meridianbet, huu ndio wakati wako! Tunakupatia Bonasi ya 3,500 Tsh papo hapo kama sehemu ya ukaribisho!


