Nyota wa Barcelona Lionel Messi yupo kwenye hatari ya kupoteza rekodi yake ya Supercopa de Espana wikiendi hii kwa mujibu wa chapisho la Marca.
Nyota huyu ambaye anajitahidi kurejea katika hali yake shwari baada ya kupata jeraha wikiendi iliyopita, anaweza kuikosa mechi ya fainali ya Supercopa de Espana dhidi ya Athletic Bilbao Jumapili.
Kama Messi akiikosa fainali hii, itakuwa ni fainali ya kwanza ambayo BArcelona wanapambana bila kuwa na Lionel Messi tangia ile ya Kombe la Dunia la Vilabu mwaka 2006, ambayo Barca walipoteza dhidi ya Internacional wa Brazil.Mesi aliikosa mechi hii pia kwa sababu ya jeraha.
Tangia wakati huo, fainali zote 27 zilizofuata Leo alihusika dimbani. Fainali yeyote bila Messi kwa mashabiki wa Barcelona ni kitu ambacho hakifikiriki na kazi kujua nini kitafuata kutokana na umuhimu wake kwa takribani fainali zote alizocheza, lakini hili linaweza likatokea Jumapili hii.
Messi alipata jeraha la paja wiki iliyopita, na amekuwa akiendelea vizuri. Licha ya wasi wasi kuwa huenda kesho ikawa vigumu kwake kucheza. Anasafiri na kikosi cha Koeman, akipewa fursa ya kujaribu kujiweka sawa tayari kwa mchezo.
MERIDIANBET INAKUPA NAFASI YA KUWA MILIONEA KWA KILA BAADA YA DAKIKA 5
Mchezo wa Keno unakupatia fursa ya kuibuka kidedea kupitia droo zinazochezwa kila baada ya dakika 5 tu!! Tunaposema Meridianbet ni nyumba ya mabingwa, tunamaanisha!!
Magdalena
Washaanza kumfanyia vitimbwi sasa
Sania
Jamani Messi
Angelina
Duuh sa itakuaje
lombo
hana jipya
Adelta
Tusubiri tuone
Sadick
Inaonekana kama Barcelona haiwezi chochote bila Messi. Hili sio jambo la afya hata kidogo
Dorophina
Pole sana messi
Ernest Kimeru
Habari Mbaya kwa Messi na wapenzi wa Barca
Lydia Emmanuel Magoti
Daah sasa itakuwaje
Issa
Mess noma
Caroline
Messi ameshuka kiwango tena
felister
sa itakuaje
Mwanahamisi
Messi noma
Sylvester
Alikua na sifa kwa muda mwingi akiwa na Barcelona na lazima tujue kwamba kila lenye mwanzo lina mwisho
Hopemwaikuka
Too bad for him
warda
Jamani atakuwa ameanza mwaka vibaya