Mkurugenzi wa klabu ya PSG Luis Ocampos amefunguka juu ya mchezaji nyota wa klabu hiyo Kylian Mbappe kuondoka klabuni hapo na kukanusha taarifa hizo.
Mkurugenzi huyo amefunguka baada ya taarifa kuibuka juu ya staa huyo kupeleka barua kwa uongozi na kutoka kuondoka klabuni hapo baad ya kudaiwa makubaliano baina ya mchezaji na viongozi wa klabu hiyo yamekiukwa ndo sababu kubwa.
Bwana Ocampos anaeleza kua ana mawqsiliano mazuri na mchezaji huyo lakini hajawahi kumuambia suala lake la kutaka kuondoka klabuni hapo “Nimekua nikiongea na Mbappe kila siku na hajawahi kuniambia anataka kuondoka hapa January” Alisema mkurugenzi huyo wa michezo klabuni hapo.
Aidha kocha wa klabu ya PSG Christopher Galtier pia ameeleza yeye bado hajapata nafasi ya kuzungumza na Mbappe kuhusuana na suala hilo mara baada ya mchezo wa jana kati yao na Benfica.
Mbappe ambae alisaini mkataba mpya miezi mitano iliyopita ya kusalia klabuni hapo na kumfanya kua mchezaji anaelipwa zaidi duniani lakini kwasasa inaelezwa hana furaha klabuni hapo na anataka kuondoka.

