Mount Kuwakosa Arsenal kwasababu ya Majeraha

Kiungo wa klabu ya Manchester United raia wa kimataifa wa Uingereza Mason Mount atawakosa Arsenal katika mchezo wa jumapili utakaopigwa katika dimba la Old Trafford.

Kocha wa Man United Eric Ten Hag leo akizungumza na waandishi wa habari ameweka wazi kua kiungo huyo hatakua sehemu ya wachezaji ambao watacheza mchezo wa Jumapili dhidi ya Arsenal kutokana na majeraha mapya ambayo ameyapata.mountMount amekua akiandamwa na majeraha mara kwa mara tangu ajiunge na klabu hiyo kwenye dirisha kubwa lililopita jambo ambalo limemfanya kukosa michezo mingi zaidi ndani ya kikosi cha Manchester United msimu huu.

Mbali na kiungo Mason Mount lakini beki Luke Shaw nae hataweza kucheza mchezo huo licha ya kuelezwa kupona majeraha yake, Hii inaonesha kua klabu hiyo itaendelea kumtumia Wan Bissaka kama beki wa kushoto kwenye mchezo dhidi ya Arsenal.mountKlabu ya Manchester United inaweza kua klabu inayoongoza kwa kukubwa na majeraha msimu huu, Kwani mpaka sasa wamesharipoti kesi za majeraha ya wachezaji hao mara 65 ndani ya msimu huu jambo ambalo linaonekana kuchangia klabu hiyo kutokufanya vyema msimu huu.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.