Mwamuzi Aliyekataa Goli la Simba kwenye Dabi ya Kariakoo Afungiwa miezi Sita

Waamuzi wasaidizi wawili wamefungiwa kufuatia makosa ya kutafsiri sheria za mpira wa miguu katika mchezo wa Dabi ya Kariakoo kati ya Simba SC na Young Africans SC uliochezwa Visiwani Zanzibar kwenye Uwanja wa New Amaan Complex. Uamuzi huo umefikiwa baada ya tathmini ya matukio kadhaa yaliyoibua mjadala wakati wa mchezo huo mkubwa wa ligi.

Mwamuzi Aliyekataa Goli la Simba kwenye Dabi ya Kariakoo Afungiwa miezi Sita

Msaidizi namba moja wa mchezo huo, Kassim Mpanga kutoka Dar es Salaam, amefungiwa kwa kipindi cha miezi sita baada ya kubainika kufanya kosa katika dakika ya 70 ya mchezo. Katika tukio hilo, alikataa bao halali la Simba akidai kulikuwa na kuotea kabla ya mpira kufungwa.

Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa

Hata hivyo, baada ya wataalamu wa sheria za mpira wa miguu kuchambua tukio hilo kwa kutumia video ya mchezo, ilibainika kuwa hakukuwa na kuotea katika tukio hilo. Matokeo yake, uamuzi wa mwamuzi huyo ulithibitishwa kuwa wa makosa na kusababisha adhabu hiyo kutolewa.

Wakati huohuo, msaidizi namba mbili wa mchezo huo, Hamdan Said kutoka Mtwara, naye amechukuliwa hatua za kinidhamu na kufungiwa kwa miezi mitatu. Adhabu hiyo imetokana na kushindwa kutafsiri ipasavyo sheria ya kuotea katika dakika ya 61 ya mchezo.

Mwamuzi Aliyekataa Goli la Simba kwenye Dabi ya Kariakoo Afungiwa miezi Sita

Katika tukio hilo, alionesha kuwa mshambuliaji wa Young Africans, Prince Dube, alikuwa ameotea wakati timu yake ikifanya shambulizi dhidi ya Simba. Uamuzi huo ulisababisha shambulizi la Yanga kusimamishwa licha ya kuwa lilikuwa linaendelea kwa hatari kuelekea langoni.

Baada ya uchunguzi wa video ya tukio hilo kufanywa na wataalamu wa sheria za mpira wa miguu, ilithibitika kuwa mshambuliaji huyo hakuwa ameotea wakati mpira unapigwa. Kutokana na makosa hayo mawili, waamuzi hao wameadhibiwa kwa mujibu wa Kanuni ya 42:1(1.8) ya Ligi Kuu inayohusu udhibiti na nidhamu ya waamuzi.

 

 

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.